Jana tarehe 29 Julai, 2014 nimefanya mahojiano katika kipindi cha
PowerBreakFast kinachorushwa na Clouds FM. Baadhi ya vyombo vya habari
vimeandika mahojiano yale. Napenda nitoe ufafanuzi kidogo kuhusu msimamo
wangu kuhusu mchakato wa Katiba.Kwanza, Mimi sijawahi kuwa UKAWA wala
kundi lolote lile katika Bunge Maalumu la Katiba isipokuwa kundi
linalotaka maridhiano. Msimamo wangu kuhusu Muungano ni Serikali Tatu
Zilizoboreshwa (S3z) ili kuwa na Muungano imara usio tegemezi wala
egemezi kwa Washirika wake. Pili, Mimi niliunga mkono ‘protest’ ya
baadhi ya Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kupinga lugha za matusi na
lugha za kibaguzi zilizokuwa zinaendelea ndani ya mkutano ule. Vilevile
niliunga mkono kwamba Rasimu inayopaswa kujadiliwa ni Rasimu iliyotokana
na Tume ya Marekebisho ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Sinde
Warioba.
Nasisitiza umuhimu wa kupata Katiba BORA itakayoimarisha DOLA ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tatu,
kwa hali ya sasa kuna mkwamo katika kupatikana kwa Katiba Bora. Mkwamo
unaotokana na kutokuwepo kwa nia ya dhati ya kupata maridhiano ya pande
zinazopingana. UKAWA hawataki mazungumzo na Viongozi wa Bunge la Katiba
badala ya kujenga maridhiano kila siku wanawabeza UKAWA jambo ambalo
kamwe haliwezi kujenga mwafaka.Ushauri wangu ni kuahirisha
mchakato mzima wa kuandika Katiba mpaka mwaka 2016 baada ya Uchaguzi
Mkuu wa mwaka 2015. Katiba ya sasa ifanyiwe marekebisho machache kama
ifuatavyo;
i) Tume
ya Uchaguzi ili iwe huru na ionekane kuwa huru, ikiwemo kuwaondoa
watumishi wa Halmashauri za Wilaya, Miji na Majiji katika kusimamia
uchaguzi
ii) Kuruhusu mgombea binafsi
iii) Kuondoa Mafuta na Gesi kama Jambo la Muungano ili Zanzibar ianze
mara moja kusimamia kwa uhuru utafutaji wa Mafuta katika vitalu
vilivyopo upande huo wa Muungano
Mkutano wa Bunge Maalumu utakaofanyika bila kuwepo kwa maridhiano
utakuwa hauna maana yeyote na itakuwa ni sawa na kupoteza muda na fedha
za walipa kodi ambazo zingeweza kununua madawa vijijini.Mimi binafsi
sitahudhuria mkutano wa Bunge Maalumu kama makundi hasimu hayatakuwa
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Profesa Lipumba Asema Hana mpango wa kuhama CUF wala kuanzisha chama Kingine ........Ataja Sababu Zilizomfanya Amkatae Lowassa08 Sep 20160
Aliyekuwa mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amesema hana mpango wa kuhamia chama choch...Read more ?
- Msajili amlima Barua Maalim Seif kuhusu sakata la Lipumba01 Sep 20160
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa nchini imemuandikia barua Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananch...Read more ?
- Breaking News: Mbowe Atangaza Kuahirisha Maandamano ya Oparesheni UKUTA Yaliyokuwa Yamepangwa Kufanyika Kesho31 Aug 20160
Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo ametangaza kusitishwa kwa maandamano ya Opare...Read more ?
- Hotuba ya Edward Lowassa alipokuwa Iringa Jana25 Aug 20160
Leo(Jana) nimewatembelea ndugu zangu wa Kilolo - Iringa kuwashukuru na kuwaeleza kuwa tu...Read more ?
- Prof Lipumba:Sihusiki na Vurugu zilizotokea Katika Mkutano wa CUF23 Aug 20160
Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF Prof.Ibrahim Lipumba amesema hausiki na fujo wala vurugu zilizotokea ...Read more ?
- Mbunge kizimbani kwa maneno ya uchochezi23 Aug 20160
MBUNGE wa Jimbo la Tanga kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Mussa Mbarouk amefikishwa katika Maha...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)













Post a Comment
Post a Comment