Home
»
SIASA
» Zitto Kabwe na Chama Chake cha ACT Wajigamba Kunyakua Majimbo Manne ya Ubunge Uchanguzi 2015
Chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT), kimesema kinatarajia kunyakuwa majimbo manne ya ubunge katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba, mwaka huu.
Kimetaja majimbo hayo kuwa ni Ubungo, ambalo linaongozwa na John Mnyika (Chadema), Kawe linaloshikiliwa na Halima Mdee (Chadema), Segerea ambalo Mbunge wake ni Makongoro Mahanga (CCM) na Kahama la James Lembeli (CCM).
Kiongozi Mkuu wa Chama hicho, Zitto Kabwe, alisema hayo katika kipindi cha Hot Mix kinachorushwa na kituo cha EATV.
Zitto aliendeleza msimamo wake wa kutogombea ubunge kwenye jimbo lake la awali la Kigoma Kaskazini.
“Nina maombi jimbo la Kahama, Kawe, Ubungo na Segerea lakini kwa kuwa ACT kinaongozwa kizalendo, tutaweka utaratibu mzuri wa kuweka wagombea kila eneo, binafsi kwa sasa siwezi kusema wapi nitagombea,” alisema.
Alipoulizwa ni eneo gani kati ya hayo aliyoyataja huduma yake inahitajika, alijibu kwa kifupi kuwa, nchi nzima ina muhitaji.
“Kabla ya kampeni kuanza wagombea wakirudisha fomu ndipo mtajua Zitto anagombea jimbo gani, lakini lazima niongozwe na chama nikagombee wapi , wanaweza kusema Zitto kagombee jimbo A,” alisema.
Aliongeza kuwa, ACT kinahitaji kujipanga kuingia kwenye mapambano ya kufyeka msitu wa siasa kwa kuwa ndani yake kuna vyama zaidi 22 na vingine vikiwa na uzoefu mkubwa kutokana na kudumu zaidi ya miaka 23.
Alisema kazi kubwa walionayo ni kukijenga chama ili kiweze kulirudisha taifa kwenye misingi ya waasisi waliyoiacha.
Aliongeza kuwa, baadhi ya watu wanamuona kama anaanza upya kwa sababu wapo wachache waliwahi kujaribu na kuishia njiani.
Alipoulizwa kuhusu wachambuzi wa siasa wanavyomchukulia hivi sasa, Zitto alisema wapo wenye mtazamo hasi na wengine chanya.
Alisema kwa wale wanaomchukulia kwa mtazamo hasi anaendelea kuwafundisha na kuwaonyesha kwamba muono wao ni tofauti wakati wale wa chanya anaendelea kuwasikiliza ili kupata muongozo zaidi kutoka kwao.
“Tukumbuke hii nchi watu wamezoea kuchukia mabadiliko angalia kwenye sanaa wakimuona Diamond amefanikiwa waanza kutoa maneno ambayo siyo, watu wanachukia mabadiliko,” alisema.
Udaku Specially Blog
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Profesa Lipumba Asema Hana mpango wa kuhama CUF wala kuanzisha chama Kingine ........Ataja Sababu Zilizomfanya Amkatae Lowassa08 Sep 20160
Aliyekuwa mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amesema hana mpango wa kuhamia chama choch...Read more ?
- Msajili amlima Barua Maalim Seif kuhusu sakata la Lipumba01 Sep 20160
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa nchini imemuandikia barua Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananch...Read more ?
- Breaking News: Mbowe Atangaza Kuahirisha Maandamano ya Oparesheni UKUTA Yaliyokuwa Yamepangwa Kufanyika Kesho31 Aug 20160
Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo ametangaza kusitishwa kwa maandamano ya Opare...Read more ?
- Hotuba ya Edward Lowassa alipokuwa Iringa Jana25 Aug 20160
Leo(Jana) nimewatembelea ndugu zangu wa Kilolo - Iringa kuwashukuru na kuwaeleza kuwa tu...Read more ?
- Prof Lipumba:Sihusiki na Vurugu zilizotokea Katika Mkutano wa CUF23 Aug 20160
Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF Prof.Ibrahim Lipumba amesema hausiki na fujo wala vurugu zilizotokea ...Read more ?
- Mbunge kizimbani kwa maneno ya uchochezi23 Aug 20160
MBUNGE wa Jimbo la Tanga kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Mussa Mbarouk amefikishwa katika Maha...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment