Wakiwa na majeruhi ya kipigo walichopata wiki mbili zilizopita kutoka kwa mahasimu wao Manchester United – Liverpool leo walisafiri mpaka jijini London kwenda kupambana na kuweka hai matumaini ya kuingia Top 4 kwa kucheza dhidi ya Arsenal.
Hata hivyo matumaini yao ya kuingia kwenye Top 4 yamezidi kupotea baada ya kukubali kupewa kibano cha magoli 4-1 kutoka kwa Arsenal.
Mpaka dakika 45 za kwanza zinamalizika ubao wa matokeo ulikuwa unasomeka Arsenal 3-0 Liverpool – Hector Bellarin, Mesut Ozil na Alexis Sanchez wakiwa wafungaji wa magoli hayo.
Kipindi cha pili Liverpool walianza kwa kumuingiza Daniel Sturridge na kufanikiwa kupata goli moja baada ya Raheem Sterling kufanyiwa madhambi na Bellarin kisha Henderson akafunga mkwaju wa penati.
Huku dakika zikiwa zinayoyoma mwanasoka bora wa mwezi March katika EPL – Oliver Giroud alifunga goli zuri kabisa na kushindilia msumari wa mwisho kwenye jeneza la Liverpool leo hii.
Kwa matokeo hayo Arsenal wamepanda mpaka nafasi ya pili kwenye ligi.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Ujumbe wa Samatta kwa Waliotamani Genk Ingepangwa Kundi Moja na Man United28 Aug 20160
Mchana wa August 26 2016 shirikisho la soka barani Ulaya UEFA lilichezesha droo ya kupanga makund...Read more ?
- Cristiano Ronaldo ashinda tuzo ya mwanasoka bora Ulaya26 Aug 20160
Mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa mwanasoka bora Ulaya. Ron...Read more ?
- Makundi ya klabu Bingwa Ulaya 2016/201726 Aug 20160
Droo ya kupanga Makundi ya klabu Bingwa Ulaya 2016/2017 ratiba kamili ya hatua ya makundi ya Uefa ...Read more ?
- MICHEZO Bilionea anayetaka kuinunua Simba, ametaja kilichomsikitisha katika mkutano wa Simba01 Aug 20160
Siku moja baada ya mkutano mkuu wa Simba kufanyika na kukubali kupitisha maadhimio ya mabadilik...Read more ?
- Gonzalo asajiliwa na Juventus kwa pauni milioni 7528 Jul 20160
Klabu ya Juventus wamekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Argentina, Gonzalo Higuain kutoka klabu...Read more ?
- Hongera Yanga kwa mlipofika, tujipange upya28 Jul 20160
Ni muda mrefu soka la Tanzania kwenye ngazi za vilabu limeonekana kuzorota kufuatia vilabu vyake k...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment