Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Wakiwa na majeruhi ya kipigo walichopata wiki mbili zilizopita kutoka kwa mahasimu wao Manchester United – Liverpool leo walisafiri mpaka jijini London kwenda kupambana na kuweka hai matumaini ya kuingia Top 4 kwa kucheza dhidi ya Arsenal.
Hata hivyo matumaini yao ya kuingia kwenye Top 4 yamezidi kupotea baada ya kukubali kupewa kibano cha magoli 4-1 kutoka kwa Arsenal.
Mpaka dakika 45 za kwanza zinamalizika ubao wa matokeo ulikuwa unasomeka Arsenal 3-0 Liverpool – Hector Bellarin, Mesut Ozil na Alexis Sanchez wakiwa wafungaji wa magoli hayo.
Kipindi cha pili Liverpool walianza kwa kumuingiza Daniel Sturridge na kufanikiwa kupata goli moja baada ya Raheem Sterling kufanyiwa madhambi na Bellarin kisha Henderson akafunga mkwaju wa penati.
Huku dakika zikiwa zinayoyoma mwanasoka bora wa mwezi March katika EPL – Oliver Giroud alifunga goli zuri kabisa na kushindilia msumari wa mwisho kwenye jeneza la Liverpool leo hii. 
Kwa matokeo hayo Arsenal wamepanda mpaka nafasi ya pili kwenye ligi.


















Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top