Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Yanga FANS
Leo APRIL 4 2015 historia imeandikwa kwenye michezo TZ, wawakilishi wetu kwenye Michuano ya Shirikisho la Soka Afrika, Yanga SC wameikamilisha kazi ya kutuwakilisha uwanjani Zimbabwe ambapo walikuwa wakipambana na timu ya nchi hiyo FC Platinum kwenye mchezo wa marudiano.

Labda matokeo ya mechi ya kwanza ambayo ilichezwa TZ kati ya timu hiyo na Yangaambayo iliibuka na ushindi wa goli 5-1 iliwafanya mabingwa hao kucheza mchezo huu kwa ujasiri mkubwa sana, huku wenzao wakijiongeza nguvu ya ziada ili wapate matokeo mazuri nyumbani kwao.
Dakika 90 zilikamilika zikaongezwa nyingine nne lakini haikusaidia kubadili matokeo hayo,FC Platinum walitoka na ushindi wa goli 1-0, lakini matokeo hayo bado yanaipa nafasiYanga kuendelea na mashindano hayo huku safari ya Platinum ikiishia hapohapo nyumbani kwao kwenye Uwanja wa Mandava.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top