Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Ligi kuu ya England imeendelea tena jioni ya leo baada ya kupisha mechi za kimataifa mwishoni mwa wiki iliyopita.
Manchester United baada ya kupata matokeo ya ushindi dhidi ya wapinzani wao wa jadi Liverpool wiki mbili zilizopita – leo hii walikuwa katika dimba lap la nyumbani kucheza dhidi ya Aston Villa.
Villa waliingia Old Trafford wakiwa na kumbukumbu ya kupata sare ya 1-1 dhidi ya United katika raundi ya kwanza ya EPL – lakini leo hii hali ilikuwa tofauti wakicheza na United ambayo ipo katika kiwango cha juu.
Matokeo ya mchezo huo ni ushindi wa 3-1 kwa vijana wa Louis Van Gaal.
Magoli ya Ander Hererra aliyefunga mawili na Wayne Rooney aliyefunga moja yalitosha kuipeleka United mpaka nafasi ya 3 katika msimu wa ligi mbele ya Man City ambao watakipiga na Crystal Palace jumatatu usiku.
Man U itakairibisha City Old Trafford wikiendi ijayo katika mchezo wa raundi ya pili ya EPL.
Matokeo mengine:
Arsenal 4 - 1 Liverpool 
Bonyeza HAPA
Everton 1 - 0 Southamton
Leicester 2 - 1 West Ham U
Swansea 3 - 1 Hull City 
West Brom 1 - 4 QPR
HT: Chelsea 1 - 1 Stoke City

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top