Home
»
Habari kimataifa
» TANZANIA TUNAENDEKEZA MAJUNGU, WENZETU INDIA WAPELEKA CHOMBO SAYARI YA MARS!
Wanasayansi wa anga za juu nchini India wanasema kuwa chombo chao cha safari za anga za juu kwa sasa kinazunguka sayari ya Mars.
Hii ndiyo mara ya kwanza kwa India kutuma mtambo wake kwenda kwa sayari hiyo, safari ambayo imepata umaarufu kutokana na gharama yake ya chini kabisa ya dola milioni 75 pekee.
India ndilo taifa la nne duniani kufaulu kufikisha chombo katika sayari ya Mars.
Mataifa mengine ambayo yamewasilisha vyombo vya utafiti wa anga za juu katika sayari hiyo ni Marekani Urusi na muungano wa mataifa ya Ulaya.
Chombo hicho ''The Mangalyaan robotic probe'' kinatarajiwa kuanza upekuzi na uchunguzi wa hali ya anga katika sayari hiyo nyekundu.
Waziri muu nchini India Narendra Modi ambaye alishuduia mafaniko ya chombo hicho kilichoanza safari yake miezi kumi iliyopita aliwapongeza wanaayansi hao kwa ufanisi huo mkubwa.
Aliwaambia kuwa mafanikio ya safari za anga za ju nchini India ni mfano mwema wa hatua ambazo taifa hilo linaweza kupiga akisema kuwa ana mpango wa kuboresha kitengo hicho.
Shirikisho la anga za mbali la Marekani NASA ambalo lilifikisha chombo chake ''Maven'' katika sayari ya Mars Jumatatu wiki hii, liliwapongeza wanasayansi wa India kwa ufanisi wao.
Kupitia kwa ujumbe wa mtandao wa Twitter NASA iliandika kuwa ''Tunawapongeza @ISRO kwa kuwasili katika sayari ya Mars. Mtajiunga na @MarsOrbiter kutathmini hali ilivyo katika sayari hiyo".
CREDIT: BBC
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Kijana Mwingine Mweusi Auawa Nchini Marekani24 Dec 20140
Eneo la tukio maandamano makubwa yametokea nchini Marekani katika mji wa St Louis yaliyosababis...Read more ?
- Wanajeshi 54 wa Nigeria Wahukumiwa Kifo kwa Kushindwa kupambana na Boko Haram.18 Dec 20140
Mahakama moja ya kijeshi nchini Nigeria imewahukumu kifo askari 54 kwa kukataa kupigana na kundi...Read more ?
- Watu 3 wauawa katika vita nchini Somalia13 Dec 20140
Mwanajeshi wa serikali ya Somali .Vita vimezuka katika ya wanajeshi wa somali na wanamgambo wa Alh...Read more ?
- Milipuko Wiliwi Yaua Watu 30 Nchini Nigeria12 Dec 20140
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({}); Waokoaji na wakazi wakikutana katika e...Read more ?
- Al Jazeera yaihusisha Kenya na mauaji ya Viongozi wa Kiislamu09 Dec 20140
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({}); Abubakar Shariff Makaburi ni mmoja wa vio...Read more ?
- Mtoto wa Malkia wa Uingereza kwa mara ya kwanza ndani ya ‘White House’ ya Marekani09 Dec 20140
(adsbygoogle = window.adsbygoogle || []).push({}); Familia ya Kifalme ya Prince Willium na...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment