Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Watafiti wa afya kupitia jarida la Addiction wamedai kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya unywaji wa pombe na aina saba za saratani.
Aidha wataalamu hao wamegundua kuwa saratani ambazo imegunduliwa zina uhusiano mkubwa na unywaji pombe ni pamoja na saratani ya mdomo na koo, saratani ya kikoromeo, saratani ya ini, saratani ya utumbo mpana, saratani ya matumbo na saratani ya matiti.
Aidha mwezi Januari mwaka huu, afisa mkuu wa afya kutoka nchini Uingereza alitoa tahadhari kuwa unywaji wa pombe kwa kiwango chochote kile kina madhara ndani ya mwili.
Mpaka sasa watu zaidi ya laki tano wanakadiriwa kufa kutokan ana ugonjwa wa saratani kwa mwaka 2012 pekee. Hata hivyo mpaka sasa bado haijabainika kibaiolojia uhusiano wa pombe na saratani inatokeaje

Chanzo: Bongo5

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
23 Jul 2016

Post a Comment

 
Top