Jose Mourinho amesisitiza kwamba hawezi kujaji wachezaji wake wa Manchester United kutokana na kipigo cha mabao 4-1 walichokipata kutoka kwa Borussia Dortmund na kusema kwamba: “Injini ilikuwepo ilikuwa ni tofauti kabisa, iliku ni kati ya Formula One against Formula Three”
“Mawazo yangu ni rahisi mno,” alisema Mourinho. “Najua kwamba wakati huu wa pre-season timu ambayo iko vizuri kwenye maandalizi lazima iwe vizuri zaidi ya rimu nyingine.”
“Hii hutokea kila mwaka. Baadhi ya timu bora hupoteza kwa magoli mengi. Nadhani hili lipo wazi kabisa. Baada ya dakika 10, tulianza kujua kwamba timu moja ilianza mazoezi siku 10 zilizopita na kucheza mchezo mmoja na nyingine ilianza mwezi mmoja uliopita na imeshacheza michezo minne. Ni rahisi mno kuona kuona utofauti wa ugumu wa mchezo na umakini wa wachezi. Kwa upande wetu ulikuwa ni mchezo mgumu sana.
Kipindi cha pili tulikuwa wazuri na kuuzoea zaidi mchezo. Nadhani matokeo ya mabao 3-2 yangekuwa sahihi zaidi ya 4-1 lakini Dortmund walionesha ubora mkubwa waliokuwa nao, kwa mchezaji mmoja-mmoja na timu nzima. Walionesha kwamba walikuwa wameshapiga hatua kubwa kwenye mazoezi zaidi yetu.
Alipoulizwa kama angewajaji wachezaji wake kutokana na mchezo ule, Mourinho akajibu: “Mimi nadhani ni muunganiko wa sababu vitu mbalimbali. Lakini kwa kuzungumzia uhalisia wenyewe, sidhani kama naweza kuwafanyia tathmini ilhali kulikuwa na utofauti mkubwa kati ya timu hizi. Kwa sasa injini zina utofauti mkubwa. Formula One dhidi ya Formular Three.
‘Kwa sasa, wapo vizuri zaidi na unaweza kuona hilo kirahisi zaidi, hivyo ni vigumu sana kuwajaji wachezaji wangu. Hata kwenye masuala kama haya, unaweza kupata wachezaji watatu, wanne au watano. Vinginevyo ni vigumu sana japo unaweza kuona ubora uliopo.”
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Ujumbe wa Samatta kwa Waliotamani Genk Ingepangwa Kundi Moja na Man United28 Aug 20160
Mchana wa August 26 2016 shirikisho la soka barani Ulaya UEFA lilichezesha droo ya kupanga makund...Read more ?
- Cristiano Ronaldo ashinda tuzo ya mwanasoka bora Ulaya26 Aug 20160
Mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa mwanasoka bora Ulaya. Ron...Read more ?
- Makundi ya klabu Bingwa Ulaya 2016/201726 Aug 20160
Droo ya kupanga Makundi ya klabu Bingwa Ulaya 2016/2017 ratiba kamili ya hatua ya makundi ya Uefa ...Read more ?
- MICHEZO Bilionea anayetaka kuinunua Simba, ametaja kilichomsikitisha katika mkutano wa Simba01 Aug 20160
Siku moja baada ya mkutano mkuu wa Simba kufanyika na kukubali kupitisha maadhimio ya mabadilik...Read more ?
- Gonzalo asajiliwa na Juventus kwa pauni milioni 7528 Jul 20160
Klabu ya Juventus wamekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Argentina, Gonzalo Higuain kutoka klabu...Read more ?
- Hongera Yanga kwa mlipofika, tujipange upya28 Jul 20160
Ni muda mrefu soka la Tanzania kwenye ngazi za vilabu limeonekana kuzorota kufuatia vilabu vyake k...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment