Home
»
general news
» Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako Aufuta Mfumo wa GPA Na Kurudisha Mfumo wa Divisheni kwa Kidato cha Nne Na Sita
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako amefuta mfumo wa matokeo ya GPA kwa wanafunzi wa kidato cha nne, sita na ualimu na kurudisha ule wa zamani wa divisheni.
Mbali na hilo, Ndalichako ameagiza kuondolewa kwa mtihani wa pili (paper two) kwa watahiniwa binafsi ambao ulianza mwaka 2014.
Katika mkutano na waandishi wa habari jana, Profesa Ndalichako alisema Serikali haitawavumilia watu ambao wanataka kuchezea elimu.
“Nilitembelea Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Januari 7, nikaagiza wanipe sababu za msingi za kutoka divisheni kuingia GPA, hadi leo wameleta maelezo bila ya sababu za msingi na maelezo yao yamejikita katika blabla ambazo hazijitoshelezi,” alisema Profesa Ndalichako ambaye katika mkutano huo aliongozana na naibu wake, Stella Manyanya na Katibu Mkuu wa Necta, Dk Charles Msonde.
Alisema kuna mgongano mkubwa katika upangaji wa GPA kwani kidato cha nne ufaulu unaanzia 3.6 -5, kidato cha sita katika daraja hilo wanaanzia 3.7 -5 wakati ufaulu kama huo kwa mafunzo ya ualimu unaanzia 4.4 -5 ambao ni mkanganyiko mkubwa unaozalisha watu wasio na ubora wa kiwango husika.
“Baadhi ya watahiniwa waliopitia katika mfumo huo na kufaulu wanaonyesha kiwango kidogo cha maarifa kuliko kiwango cha ufaulu,”alisema.
Alisema kuwapo gredi E kwenye alama za ufaulu wakati haihesabiki katika upangaji wa GPA, kunawafanya watahiniwa waliopata E kujiona wako bora kuliko wenye D mbili na F zote ambao wanahesabiwa wamefaulu.
Alisema Necta imetoa maelezo mengi ambayo yameonekana hayana uhalisia wala wa kukamilisha sababu badala yake wamejikita katika visingizio.
Alisema Necta walimweleza kuingia katika mfumo huo ilikuwa ni maoni ya wadau lakini alipowauliza ni wadau kiasi gani na mikutano hiyo ilifanyikia wapi, hawakuwa na majibu na hakuna hata mkutano ambao uliwahi kufanyika.
“Jambo jingine lazima mkumbuke kuwa, mfumo huu haujaenda hata kwa kamishna wa elimu kupata kibali, ndiyo maana wadau waliniambia kuwa nisingetoa siku saba badala yake ningeufuta mara moja,” alisema Ndalichako.
Alipinga madai kwamba uliruhusiwa na Serikali, akisema ulianza kutumika tangu 2014 wakati maagizo ya Serikali Mtandao (EG) yalieleza kuwa kila kitu kianze kutumika Juni 16, mwaka huu.
Alisema alidanganywa kwa kuambiwa wizara iliagiza wakati amebaini kuwa wizara ilipitisha kanuni za mitihani Oktoba 28, 2015 na kuingiza katika gazeti la Serikali Novemba 6 mwaka jana ikiwa ni miaka miwili tangu mfumo wa GPA uanze kutumika.
Kwa upande wa watahiniwa binafsi, alisema kuanzia sasa hakutakuwa na mitihani miwili ambayo mmoja ulikuwa ni kwa ajili ya upimaji endelevu, hivyo watahiniwa watafanya mtihani mmoja tu.
Hata hivyo, Dk Msonde alisema watahiniwa binafsi wa sasa watasahihishiwa mitihani yao kwa mfumo wa mitihani miwili kwa kuwa walishafanya.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Jamaa Aliyejitosa Zoo Aliwe na Simba Laivu Alikuwa Anadai Mwisho wa Dunia Umefika...23 May 20160
Inasikitisha kwakweli, ameokolewa.... na simba walioanza kumla waliuwawa. aliingia kwenye jumba ...Read more ?
- Watumishi HEWA Waziponza Benki.......Benki za Dar es Salaam Zalimwa Barua Kurejesha Mamilioni ya Shilingi23 May 20160
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametoa siku 21 kwa benki zilizokuwa zikitumika kuwek...Read more ?
- Waziri Nchemba Afanya Ziara Ya Kushtukiza Saa Saba Usiku Machinjio Ya Ukonga Mazizi Na Kufukuza Viongozi Wote Wa Machinjio12 Feb 20160
Waziri wa Kilimo na Mifugo Mwigulu Nchemba amefanya ziara ya Kushtukiza saa saba usiku...Read more ?
- Askofu Gwajima, Sheikh Wa Mkoa Dar Wakwama Kumjulia Hali Mufti12 Feb 20160
Jopo la Madaktari wanaomtibu Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir wamezuia ...Read more ?
- Siku 100 za Rais Magufuli: Hospitali Ya Muhimbili Yang'aa, Mapato Yapaa na Upatikanaji wa Dawa Waongezeka Kwa Asilimi 9611 Feb 20160
HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili (MNH) iliyopo jijini Dar es Salaam imesema ndani ya siku 100 z...Read more ?
- Lowassa Atakiwa Kuvisaidia Vyombo Vya Dola Kukabiliana na Tishio La Kundi la al Qaeda Kuingia Nchini10 Feb 20160
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed Aboud Mohamed amemtaka Wa...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment