Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Leo ilikuwa Mwenyekiti wa CUF Prof. Ibrahim azungumze na Wanahabari asubuhi, ila mkutano huo umehairishwa hadi siku nyingine tena.
  
Wanachama wa chama cha wananchi CUF walizingira ofisi za chama hicho wakiongozwa na wazee wakitaka kujua hatima ya mwenyekiti wao Prof.Ibrahim Lipumba aliyedawai kutaka kujiuzulu.
Magdalena Sakaya alipoulizwa Prof. Lipumba alitaka kuzungumza nini amejibu hata  wao hawajui kitu alichotaka kuwaambia wananchi  
  
Magdalena alisema sababu kubwa ya kusitishwa mkutano  huo ni kuwa Wazee wa CUF wametaka kujua kwanza ni kitu gani Mwenyekiti anataka kuongea.
  
Wananchi nje ya ofisi za CUF walikuwa wanashangilia wakiimba kwa kusema..... "Si mnaona, muziki wa Lipumba kuuzima hamuwezi"
 
Mmoja wa Wananchi waliokuwa wanashangilia alisema wamefurahia kwakuwa wanaamini Mwenyekiti wao Lipumba hatajiuzulu na yuko na wananchi. 

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top