Na Makongoro Oging’
Kuna taarifa kwamba kumbe askari magereza mstaafu wa Gereza la Dondwe,Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani (jina linahifadhiwa) anadaiwa kuhusika katika zoezi nzima la utoaji wa mafunzo ya kijeshi kwa watu waliovamia Kituo cha Polisi Stakishari jijini Dar es Salaam Julai 12,mwaka huu.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili unaonesha kwamba askari huyo anatajwa kuhusika kutoa mafunzo ya kijeshi na mbinu za medani kwa watu walioshiriki kitendo cha kinyama cha kuvamia kituo, kuiba silaha na kuua raia na askari.
Mwandishi wetu alielezwa na vyanzo makini vya habari kwamba askari huyo alikuwa akitoka kijijini kwao ambacho kipo mbali na makazi ya wanaodaiwa wahalifu wa tukio hilo na kuja kwenye ngome hiyo kwa ajili ya kutoa mafunzo.
“Alikuwa akijidai kuja kwenye ibada lakini alikuwa akipita nyumba nyingi za ibada, kitu kilitotushangaza wengi kwani hata kama mvua ikinyesha, hakukosa kwenda kwenye ngome ya wahalifu wale.
Imeelezwa kwamba askari huyo alikuwa akiwatembelea watuhumiwa hao huko porini kwenye ngome yao bila vikwazo lakini raia wa kawaida hawakuruhusiwa kwenda au kupita maeneo hayo jambo liliokuwa likileta maswali mengi juu ya uhusiano wa askari huyo na watuhumiwa hao.
Hivi karibuni wananchi wa Kijiji cha Mandikongo, Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani walipokuwa wakiishi watuhumiwa hao wa mauaji wa Polisi wa Kituo cha Stakishari walikaa katika mkutano kujadili kuhusu suala la ulinzi na usalama, wakakubaliana kwa pamoja kushirikiana na polisi na vyombo vyote vya usalama kuwasaka waliohusika na tukio hilo waliokuwa wakiishi katika pori la kijiji hicho.
Hata hivyo, wananchi hao walisema askari huyo mstaafu wa magereza lazima asakwe na kukamatwa ili ahojiwe na vyombo vya serikali kuhusu urafiki wake na watuhumiwa hao ambao kwa sasa wamekimbia na familia zao na hawajulikani walipo.
“Unajua huyu askari tuna wasiwasi naye maana angekuwa mtu mzuri angeweza kutoa taarifa kwa vyombo vya dola kuhusu kikundi hicho hatari,” alisema mwanakijiji mmoja wa kijij hicho ambaye hakupenda kuandikwa jina gazetini.
Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mandikongo, Issa Said Mchalaganga alisema kwamba kamati ya ulinzi na usalam kijijini hapo wamedhamiria
watuhumiwa wote wanapatikana pamoja na silaha nzito za kivita walizokimbia nazo.
Watuhumiwa saba wanaosadikiwa kuhusika katika uhalifu mbalimbali likiwemo tukio la Stakishari hawajapatikana na vyombo vya dola vinaendelea kuwasaka.
Polisi hivi karibuni walisambaratisha kambi ya kikundi hicho na kufanikiwa kumkamata mtu mmoja, bunduki 15 na fedha shilingi milioni 170 zilizochimbiwa chini katika kambi ya watuhumiwa hao.
Polisi wanne na raia watatu waliuawa katika uvamizi wa Kituo Kikuu cha Polisi Stakishari cha Wilaya ya Kipolisi Ukonga, Julai 12, mwaka huu na watuhumiwa hao wanadaiwa kuhusika na uvamizi huo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, SACP Lucas Mkondya alipohojiwa alisema anaendelea kuwasaka watuhumiwa.
“Nawaomba wananchi kutoa taarifa kituo chochote cha polisi, vyombo vya usalama au kwa wenyeviti wa serikali ya mitaa wakiwaona watu wanaowatilia shaka,” alisema.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- BREAKING NEWS: Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha ametangaza rasmi tarehe ya kurudiwa kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar22 Jan 20160
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha ametangaza rasmi tarehe ya kuru...Read more ?
- Rais Dkt. Magufuli Amteua Jakaya Kikwete Kuwa Mkuu Wa Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam.21 Jan 20160
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Rais Mstaafu wa awamu ...Read more ?
- JANUARY MAKAMBAASHANGAZWA NA HAYA MAGAZETI MATATU KUHUSU LOWASSA02 Sep 20150
Naibu waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba ameonesha kushangazwa na mfa...Read more ?
- Polisi Yakamata Majambazi 38 Yakiwa na silaha Nzito pamoja na Milioni 170......Majambazi hayo yanadaiwa na mafunzo ya Kijeshi01 Sep 20150
Jeshi la Polisi limewakamata watu 38 wanaotuhumiwa kuwa ni majambazi ambao pia wamepatiwa mafun...Read more ?
- Wananchi Wafunga Barabara Baada ya Gari la Polisi Kugonga Wanafunzi wawili31 Aug 20150
Wananchi wa eneo la Misugusugu Wilayani Kibaha Mkoani Pwani hii leo wamefunga barabara baada ya...Read more ?
- Hali Tete Bunda, Viongozi CHADEMA Wajiuzulu...Kisa Ester Bulaya22 Aug 20150
SIKU chache baada ya mgombea ubunge wa Jimbo la Bunda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maend...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment