Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Watu kadhaa wanao daiwa kuwa ni majambazi jana  walivamia Benki ya NMB tawi la Mkuranga mkoani Pwani na kupora fedha kisha kumuua askari mmoja na kutokmea kusikojulikana.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jafary Mohamed alithibitisha jana  jioni  kupata taarifa za tukio hilo.
 
“Taarifa hizo nimezipata kuwa watu hao wanaodhaniwa majambazi wamevamia  Benki ya NMB, Mkuranga na kupora fedha ambazo kiasi chake bado hakijafahamika kisha kumuua askari mmoja aliyekuwa nje ya uzio wa eneo hilo la benki," alisema Jafary  .
 
Hata hivyo alisema askari aliyeuawa   hakuwa kazini ila walinzi wote wa benki wapo salama na silaha zao hazikuchukuliwa.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
27 Jun 2015

Post a Comment

 
Top