MAMA wa mtoto aliyeibwa kabla hajatimiza mwezi tangu azaliwe, Fatuma Bakari ameieleza Mahakama ya Wilaya ya Ilala jinsi mtoto huyo alivyoibwa na mshtakiwa Neema Patrick.
Shahidi huyo na mwingine walitoa ushahidi wao jana mbele ya Hakimu Adelf Shachore kwa kuongozwa na Wakili wa Serikali, Anunciata Leopold.
Awali mashahidi hao walikuwa watano ambao walifika mahakani kwa ajili ya kutoa ushahidi, lakini Wakili Leopold, alidai kuwa kwa mujibu wa shtaka hilo waliotakiwa kutoa ushahidi walikuwa wawili tu.
Wakitoa ushahidi wao mashahidi hao ambao ni Fatuma Bakari na Zainabu Said, wote walikiri juu ya mtuhumiwa kufanya kitendo hicho cha kuiba mtoto.
“Ni kweli siku ya tukio ambayo ni mwezi machi mwaka huu, mtuhumiwa alinisindikiza hospital nilipokuwa naumwa jino, kutokana na hali niliyokuwa nayo mtuhumiwa aliniomba anibebee mwanangu (Ibrahm Abdalah, ambaye hajatimiza hata mwezi) lakini mara baada ya kufika hospital maeneo ya Mbagala, Dar es Salaam, alishushuka haraka na kukimbia na mwanangu,” alidai Shahidi huyo.
Awali mashahidi hao walitakiwa kuwa watano lakini wakili wa serikali alipinga kutoa utetezi wao, hivyo mashahidi watatu walibaki ushahidi wao utasikilizwa Juni 24 mwaka huu.
Mtuhumiwa huyo anadaiwa kumwiba mtoto huyo maeneo ya Mbagala Machi 3 mwaka huu ambapo alikuja kukamatwa baad ya wiki mbili maeneo ya Ukonga Banana akiwa na mtoto huyo, mtuhumiwa huyo yuko nje kwa dhamana.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 12011 Sep 20160
Tetemeko la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nc...Read more ?
- Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.09 Sep 20160
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao uliku...Read more ?
- Polisi Washuhudia Majambazi Yakitwangana Risasi.......Zakamatwa Shehena za Silaha na Vifaa vya Uhalifu06 Sep 20160
WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wa kutumia silaha, ambao wamehusika kufanya matukio ...Read more ?
- Askari Magereza Atiwa Mbaroni Kwa Kuingia Wodini Akiwa Amelewa na Kisha Kuanza Kufyatua Risasi28 Aug 20160
POLISI mkoani Rukwa inamshikilia askari Magereza, Cleophas Chapaulinge kwa kosa la kulewa na k...Read more ?
- Polisi Mwingine Auawa Kwenye Mapambano Makali na Majambazi Huko Mkuranga27 Aug 20160
Ilikuwa ni kama filamu ya askari na maadui wakati askari wa Jeshi la Polisi walipopambana na wat...Read more ?
- RC Makonda: Polisi Mkikuta Mtu Yeyote Msituni Pigeni bila Huruma.......Haki za binadamu Wakiwauliza Waambieni waje Kwangu26 Aug 20160
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameliagiza Jeshi la Polisi kuwagonga na kuwapiga wah...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment