March 17, 2025 02:10:48 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
STAA wa filamu Bongo, Kajala Masanja, kupitia akaunti yake ya Instagram hivi punde amesema maisha yanaendelea ikiwa ni siku mbili baada ya kupigwa chupa na mtu asiyemfahamu usiku wa kuamkia Jumatatu akiwa klabu wakati alipokwenda katika shoo ya kumchangia mke wa Mabeste, Maisha Club

Kajala alieleza kuwa tukio hilo lilitokea wakati akijiandaa kutoka Maisha Club ambapo ghafla akiwa kwenye ngazi alirushiwa chupa kichwani iliyopelekea kuanguka kutoka kwenye ngazi hadi chini na kusaidiwa na wasamalia wema waliompeleka Hospitali ya Mwananyamala ambapo alishonwa kwenye jeraha alilolipata.

Staa huyo aliongeza kuwa mtu aliyempiga chupa ni mwanaume na tayari yupo mikononi mwa polisi japo kabla ya tukio hilo alikuwa  hamjui na wala hajawahi kumuona mtu huyo.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
12 May 2015

Post a Comment

 
Top