Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Ripoti yataja mikoa 7 yenye maendeleo duni ya watu Tanzania.

DODOMA, KIGOMA, SINGIDA, KAGERA, TABORA, SHINYANGA na PWANI ndio mikoa inayoongoza kwa maisha duni ya watu Tanzania

Hayo yamo katika ripoti iliyozinduliwa Ijumaa na serikali, ripoti hiyo pia imeitaja mikoa inayoongoza kwa hali bora za maisha ya watu Tanzania kuwa ni:
 DAR ES SALAAM, ARUSHA, KILIMANJARO, IRINGA, RUVUMA, MBEYA and TANGA.

Vigezo vilivyotumika katika utafiti uliozaa ripoti hiyo ni, wastani wa muda wa kuishi (Life expectancy, max 83.6 - min 20), expected years of schooling, upatikanaji wa maji safi na salama, umeme, lishe, vifo vya mama wajawazito na watoto, maendeleo ya jinsia.

Vigezo vingine ni, mazingira, kipato, umaskini, uhuru na upatikanaji wa mahitaji ya msingi kama chakula, maji na nyumba.

Utafiti huo ulifanywa na Economic & Social Research Foundation (ESRF) kwa kushirikiana na;
- National Bureau of Statistics (NBS).
- The Office of the Chief Government Statistician of Zanzibar.
- The Department of Economics of the University of Dar es Salaam.
Na kudhaminiwa na UN.

Source; The Citizen

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top