Mchezaji mkongwe wa Arsenal, Thiery Henry amefichua kuwa ndoto yake kuu ni kumrithi kocha wa timu hiyo Arsene Wenger katika klabu hiyo.
Mchezaji huyo wa zamani ambaye ndiye anayeongoza kwa idadi ya mabao katika klabu hiyo akiwa na magoli 228, aliripotiwa kupewa nafasi ya kuanza kufundisha soka katika chuo cha ukufunzi wa soka katika klabu hiyo mapema mwezi huu.
Raia huyo wa ufaransa amekiri kwamba ana mipango ya kumrithi Wenger wakati kocha huyo atakapoamua kustaafu.
“Sijui ni kwa muda gani Wenger anataka kuendelea kuwa kocha wa Arsenal, lakini ni sharti niwe mzoefu wa kutosha kuchukua wadhifa huo,kuwa kocha wa Arsenal ni ndoto yangu kubwa,lakini nafaa kujifunza mwanzo,hicho ndicho kitu muhimu,”-Thiery
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment