Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
MWIGIZAJI na msanii wa Bongo Fleva, Baby Joseph Madaha, amesema anatamani kuitwa mama kama ilivyo kwa wanawake wengine wenye watoto.


Akizungumzia swala hili, Baby Madaha, alisema amepanga kufanikisha ndoto zake za kuwa mama mwaka huu. “Kiukweli natamani sana kupata mtoto, nafarijika nikisikia na kuona wenzangu wanaitwa mama, ni jambo la busara na kumuomba Mungu ili litimie,” alisema Baby Madaha.

Madaha alisema wasanii wengi wamefululiza kuzaa jambo ambalo linapendeza katika jamii, lakini uamuzi wake si wakufuata mkumbo kama ambavyo wengi watafikiria.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
06 Feb 2015

Post a Comment

 
Top