Home
»
Matukio
» Watu 2 wamefariki dunia papo hapo na wengine 44 kujeruhiwa kwenye ajali ya basi mkoani Dodoma.
Watu wawili wamefariki dunia papo hapo na wengine 44 kujeruhiwa baada ya basi la kampuni ya kidia one lililokuwa likitokea jijini Dar es Salaam kuelekea jijini Mwanza kugongana uso kwa uso na lori la mizigo lililokuwa likitoka Dodoma kwuelekea Morogoro katika kijiji cha vikonje kata ya mtumba nje kidogo ya mji wa Dodoma.
ITV ilifika eneo la ajali ambapo mashuhuda wa ajali hiyo akiwemo dereva msaidizi wa basi aliyejitambulisha kwa jina moja la Makubeli akisema chanzo cha ajali hiyo ni baada ya basi kuharibika mfumo wa breki na kumshinda dereva mwenzake kauli inayopingana na mmoja kati ya abiria aliyekuwemo kwenye basi hilo ambaye anadai chanzo ni mwendo kasi ambapo dereva wa basi alikuwa akijaribu kulipita basi jingine lililokuwa mbele yao bila tahadhari na ghafla akakutana uso kwa uso na lori.
Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Sasp David Misime amesema chanzo cha ajali kimetokana na dereva wa basi hilo lenye namba za usajili T 663 AXL aina ya Scania alipokuwa akijaribu kulipita gari lingine bila kuchukua tahadhari na kukutana uso kwa uso na lori lenye namba za usajili T 496 CFG likiwa na tela namba T 576 AXZ ambapo watu wawili waliofahamika kwa majina ya Fadhili Saidi dereva wa lori na Chogo Chigunda utingo wa basi wakafariki dunia.
Kwa upande wake mganga mkuu wa hospitali ya mkoa wa Dodoma Dk Nasoro Mzee amethibitisha kupokea maiti hizo mbili na majeruhi 44 ambapo 16 wametibiwa na kuruhusiwa huku wengine 27 wakilazwa.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 12011 Sep 20160
Tetemeko la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nc...Read more ?
- Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.09 Sep 20160
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao uliku...Read more ?
- Polisi Washuhudia Majambazi Yakitwangana Risasi.......Zakamatwa Shehena za Silaha na Vifaa vya Uhalifu06 Sep 20160
WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wa kutumia silaha, ambao wamehusika kufanya matukio ...Read more ?
- Askari Magereza Atiwa Mbaroni Kwa Kuingia Wodini Akiwa Amelewa na Kisha Kuanza Kufyatua Risasi28 Aug 20160
POLISI mkoani Rukwa inamshikilia askari Magereza, Cleophas Chapaulinge kwa kosa la kulewa na k...Read more ?
- Polisi Mwingine Auawa Kwenye Mapambano Makali na Majambazi Huko Mkuranga27 Aug 20160
Ilikuwa ni kama filamu ya askari na maadui wakati askari wa Jeshi la Polisi walipopambana na wat...Read more ?
- RC Makonda: Polisi Mkikuta Mtu Yeyote Msituni Pigeni bila Huruma.......Haki za binadamu Wakiwauliza Waambieni waje Kwangu26 Aug 20160
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameliagiza Jeshi la Polisi kuwagonga na kuwapiga wah...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment