Baba mzazi wa Dully Sykes, Mzee Ebby Sykes amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 62. Angetimiza miaka 63 February 24.

Mtoto wake wa kike aitwaye Raya Sykes amethibitisha taarifa hizo kwenye mtandao wa Instagram.
“Mungu akulaze mahali pema peponi baba angu mm nilikupenda lakin mungu alikupenda zaid nasikitika nipo mbali sitaweza kukuzika!ulikua ni mtu mwenye upendo na kila mtu alikupenda nakupenda sana baba angu R I P dady nitakukumbuka milele daima,” ameandika Raya.
Bado hakuna taarifa rasmi za sababu za kifo cha Mzee Sykes. Sykes alikuwa muimbaji na mpiga gitaa mashuhuri na ndiye anayedaiwa kumfundisha mambo mengi ya muziki mwanae Dully.
“Uncle Ebby Sykes i love u…. in life and in death…'” ameandika mpwa wake, Basillah Sykes.
Mzee Sykes alizaliwa tarehe 24 February, 1952.
Mungu ailaze roho yake mahali pema.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment