March 19, 2025 08:45:06 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Mtoto wa miaka 12 mkazi wa Mkoa wa Geita ametimuliwa nyumbani na mama yake mzazi na kutakiwa kwenda kuishi maisha ya kujitegemea baada ya kuunguza mboga jikoni.
Mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya Msingi Karangalala ameamuriwa na mama yake kufanya hivyo baada ya mama yake Helena kumwachia jukumu la kupika mboga Novemba mwaka jana lakini mboga hiyo iliungua.
Baada ya kuunguza mboga hiyo,mama huyo alimpiga mwanaye kabla ya kumpa masurufia na kumkabidhi chumba tayari kwa kuanza maisha.
Mtoto huyo alisema mama yake amekua na tabia ya kumpiga mara kwa mara kiasi cha kusababisha mwili wake kuwa na alama za viboko.
“Sifahamu kwa nini mama yangu huwa ananipiga kiasi hiki,inawezekana kwa kuwa na yeye alilelewa na mama wa kambo aliyekua anampiga hivi”alisema mtoto huyo.
Chanzo:-Mwananchi

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
08 Jan 2015

Post a Comment

 
Top