Michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya imeendelea usiku huu ikiwa kwenye mzunguko wake wa mwisho wa hatua ya makundi .
Katika michezo iliyopigwa hii leo timu ya Arsenal toka England ilifanikiwa kushinda kwenye mchezo wake dhidi ya Galatasaray ya Uturuki kwa matokeo ya 2-4 katika mchezo uliopigwa huko Istanbul.
Arsenal ilifunga mabao yake kupitia kwa Aaron Ramsey na mshambuliaji raia wa Ujerumani Lukas Podolski ambapo kila mmoja alifunga mabao mawili .
Katika mchezo mwingine wa kundi D wawakilishi toka ujerumani Borrusia Dortmund walibanwa mbavu wakilazimishwa sare ya 1-1 katika mchezo dhidi ya Anderlecht ya Ubelgiji.
Matokeo haya yanamaanisha kuwa timu za Arsenal na Borrusia Dortmund zimefanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora ambapo Dortmund wamefuzu kama washindi huku Arsenal wakishika nafasi ya pili .
Katika michezo mingine iliyochezwa usiku huu Real Madrid walifanikiwa kushinda mchezo wao wa 19 mfululizo katika mashindano yote wakiwafunga Ludogorets toka Bulgaria 4-0 .
Wafungaji wa Real kwenye mchezo huo walikuwa Cristiano Ronaldo , Gareth Bale , Alvaro Arbeloa na Alvaro Medran .
Ushindi huu umewafanya Real wafuzu hatua ya 16 bora kwa kishindo wakiwa wamekusanya pointi 18 baada ya kushinda michezo yote 6 ya kundi lao .
Liverpool ambayo ilikuwa nyumbani ikicheza na Fc Basle iliambulia sare ya 1-1 matokeo ambayo yalikuwa na faida kwa wapinzani wao ambao wanaungana na Real Madrid kufuzu hatua ya kwanza ya mtoano.
Katika michezo mingine Juventus na Atletico Madrid walitoka sare ya bila kufungana , Olympiakos wakawafunga Malmo 4-2 , Benfica na Bayer Leverkusen nazo zikatoka sare ya 0-0 , huku As Monaco ikishinda dhidi ya Zenith St Petersburg kwa matokeo ya 2-0 .
Kwa matokeo haya timu za Juventus , Atletico Madrid , Monaco na Bayer Leverkusen zinaungana na Arsenal , Dortmund , Real Madrid na Fc Basel kufuzu hatua ya 16 bora .
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Ujumbe wa Samatta kwa Waliotamani Genk Ingepangwa Kundi Moja na Man United28 Aug 20160
Mchana wa August 26 2016 shirikisho la soka barani Ulaya UEFA lilichezesha droo ya kupanga makund...Read more ?
- Cristiano Ronaldo ashinda tuzo ya mwanasoka bora Ulaya26 Aug 20160
Mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa mwanasoka bora Ulaya. Ron...Read more ?
- Makundi ya klabu Bingwa Ulaya 2016/201726 Aug 20160
Droo ya kupanga Makundi ya klabu Bingwa Ulaya 2016/2017 ratiba kamili ya hatua ya makundi ya Uefa ...Read more ?
- MICHEZO Bilionea anayetaka kuinunua Simba, ametaja kilichomsikitisha katika mkutano wa Simba01 Aug 20160
Siku moja baada ya mkutano mkuu wa Simba kufanyika na kukubali kupitisha maadhimio ya mabadilik...Read more ?
- Gonzalo asajiliwa na Juventus kwa pauni milioni 7528 Jul 20160
Klabu ya Juventus wamekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Argentina, Gonzalo Higuain kutoka klabu...Read more ?
- Hongera Yanga kwa mlipofika, tujipange upya28 Jul 20160
Ni muda mrefu soka la Tanzania kwenye ngazi za vilabu limeonekana kuzorota kufuatia vilabu vyake k...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment