Kabla ya mechi ya ‘Nani Mtani Jembe’ kati ya Yanga na Simba mashabiki wa timu hizo mbili ambao ni wasanii wa filamu, Vicent ‘Ray’ Kigosi na JB walipinga yoyote atakayefungwa atavaa jezi ya mwenzake na kumkabidhi zawadi ya shilingi milioni 1.
Ray ambaye ni shabiki wa Yanga itambidi avae jezi ya Simba pamoja na kumkabidhi JB kiasi hicho cha fedha kutokana na makubaliano hayo baada ya Simba kuichapa Yanga mabao 2-0.
Kabla ya mechi kuanza JB aliandika kwenye Instagram kuwa:TUMEKUBALIANA na Ray thegreatest kuwa nikifungwa navaa jezi ya yanga na nampatia 1M.Na yanga ikifungwa anavaa jezi ya mnyama na ananipa1m.Naamini timu yangu haitaniangusha, winga okwi winga sserunkuma aaaaaah hata mimi nafunga.
Ungana nasi katika Facebook na Umechekeshwa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro








Post a Comment
Post a Comment