June 14, 2025 07:06:20 PM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Inakuwaje wanangu? Mishe zikoje kitaa hiyo? Ebana homa ya kitu cha holidei ikoje? Kama ulikuwa hujasanuka dheni nikunyakishe kwamba ni kitu cha bethidei ya Yesu so kuibuka chachi kwa wale Wakristo ndo mpango mzima dheni ukiibuka kitaa ndo bata la kufa mtu bati pliizi liwe aste-aste chaliiangu.

Ebana eee…si tupo mapumziko ya holidei so masti tukutane na vichwa vya longi taimu na mastori moo ya mwaka mzima yagongwe ileile. Unajua hapo kati yanakrosi maishu kibwena so masti michongo nayo iwe kibao.
Oyo…sijafogeti kuwapa mashavu. Tulia mabigi apu yapo dauni endelea kuperuzi.
Huku na huku baba la baba nikamingo na mwana wa kitambo kinoma. Jamaa anaanza kudropisha limkasa lake limoko lililomkuta mwaka huu unaoelekea kwa fasi ya ukingoni.

Mzazi jembe anakwenda kwa neimu moko la Tizo. Jamaa anafunguka kuwa mwanzoni mwa mwaka huu alijikuta akifoli kwenye malavu na mtoto mmoko mkareee…yaani mbebiz wa ukwehe kabisa.
Selaa katika kumchunguza yule shori akagundua ni mkidi wa taita mmoko mwenye mabovu hatari tauni kwa fasi ya Bongo tambarare.

Mwanangu anakuteli kuwa hakuwa na maujanja so akajikuta akimlavu, kumtrasti na kumpa laifu lake lote. Si unajua zile za mahaba niteketeze?Kuna wana wanadai eti mashori ticha wao ni mmoko. Huwezi kubilivu, pamoko na selaa kujitoa fahamu na kumkea kwa kila kitu bati mwisho wa dei alimchiti na kwenda kwa kichwa kingine ambacho nacho ni mkidi wa taita pia.
Si unajua auti za familia bora? Huko ndiko walikomiti na kuanza kumingo. Ujue wana viwanja vyao vinaitwa viota vya raiti pipo!Asikwambie kichwa ishu hiyo ilimuuma kachaa wangu kiasi cha kuchizika kabisa. Pipo wakaamini kuwa mwanangu hazimtoshi kichwani.
Deizi zikakrosi fasta kinoma, jamaa yangu akajikuta akijenga bonge la chuki kwa shori yeyote aliyekrosi machoni mwake.Chalii yangu alipokaa taimu ndefu akaona isiwe kitu. Akaamua kuchepukia kwenye tabia mbaya na denja kinoma ya kwenda kubeba chipsi funga. Umenisoma? Chipsi funga ni wauza sukari au machangu.
Kwenye kuchukua madadapoa huko ndiko kulikuwa na bigi problemu. Kaka mkubwa alikutana na dadapoa mkare kinoma. Alikuwa ni shori ambaye yuko diferenti kabisa na makiksi wengine wa tauni.
Mbali na ubora wake bati alikuwa na uzuri f’lani hivi na sura bomba yenye bonge la tabasamu. Shukrani kwa uumbaji wa Saa Godi.

Mwanangu anakwambia shori kama yule hakustahili kufanya ile bizinesi haramu ya kuuza bodi kozi kwa mwanaume yeyote alionekana anafaa kuolewa na kuwekwa ndani.Dah! Kwa uzuri huo na kumwamini shori, jamaa akaingia kichwakichwa bila kinga.
Miezi bee baadaye msela wangu alipokea mastori kuwa mtoto mzuri kadedi aisee arifu!
Mzazi jembe alipofuatilia alinyetishiwa kuwa yule mbebi alidedi kwa ngoma. Imajini ungekuwa wewe ndo msela ingekuwaje?

Alichokifanya msela wangu ni kwenda kupima dheni majibu hayakudanganya kozi mwanangu alikuwa amekanyaga miwaya. Kwa kuwa hakuwahi kuruka na shori mwingine tofauti na yule mbebiz dheni akahitimisha kuwa alichukua kwa chipsi funga.
Unajua kilichofuata ni nini? Tunapopiga mastori hapa msela anaishi kwa mahopu tu bati kama akijilinda anaweza kusavaivu zaidi kozi wapo watu kibwena wanaodedi deile kwa magonjwa mengine.
Ebana mmenisoma? Wanangu kuwa na bucha siyo rizoni ya kula nyama deile. Samu taimu lazima kuangalia nyama hiyo haina madhara kwa afya yako? Jitunze! Acha kuendeshwa na stimu za tamaa za mwili.

Mazee naomba niwape bigi apu sana wanangu tuliokuwa tunachatichati na kushea aidia hapa jamvini kwa mwaka mzima. Wanangu wa Roki Siti, Green Siti, Moro-Tauni, A-Town, Dom Siti, Tanga Moko, Wagumu Siti na kila kona ya Bongo. Sharauti nyingine neksti wiki. Ama nini? Nduki!

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
25 Dec 2014

Post a Comment

 
Top