Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Maiti  kumi na wawili   wanaosadikiwa  wame kufa maji   katika ajali ya  boti  iliyotokea wiki moja iliyopita Mashariki  ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya  Kongo  katika Ziwa Tanganyika wameonekana katika ufukwe wa  Ziwa Tanganyika Mkoani Kigoma .

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma  Luteni Kanali  mstaafu Issa Machibya amesema maiti hizo zimeonekana jana  wakielea  katika katika kijiji cha Kalilani ,  tarafa ya Buhingu  Wilayani  Uvinza.
Amesema kwa kushirikiana na ubalozi mdogo wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya  Kongo uliopo Kigoma, maiti hao ambao wamekwishaopolewa wa tazikwa leo katika kijiji hicho.
Kwa upande wake , Mganga Mkuu wa  Mkoa  wa Kigoma Dkt.Lenard Subi am esema kabla ya kuzikwa maiti hao watafanyiwa utambuzi wa kisayansi.
Tarehe  14 mwezi huu Boti inayoitwa  MV.Mutambala ya Jamhuri ya  Kidemokrasi  ya Kongo inayofanya safari zake  Mashariki  mwa nchi hiyo katika  Ziwa Tanganyika ilizama na kusababisha vifo vya watu  zaidi ya  120  na wengine 221 wameokolewa.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top