July 9, 2025 05:28:38 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Manchester United baada ya kushinda mechi 6 mfululizo katika ligi hiyo, leo walisafiri mpaka Villa Park kwenda kucheza na Aston Villa.
Matokeo ya mchezo huo ni Man United kusimamishwa kasi yao baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na vijana wa Paul Lambert.
Christian Benteke alianza kuifungia goli Villa katika dakika za mwanzo za kipindi cha kwanza baada ya kumhadaa beki wa United Jonny Evans na kupiga shuti ambalo De Gea aliliangalia tu likiingia golini.
Kipindi cha pili United walirudi kwa kasi na kufanikiwa kupata goli la kusawazisha kupitia Radamel Falcao aliyeruka juu na kuunganisha krosi ya Ashley Young.
Pamoja na timu zote kujaribu kupata goli la ushindi lakini mpaka refa anamaliza mechi hiyo ubao wa matokeo ulionyesha Villa 1-1 Man United.
IMG_0116.JPG

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
20 Dec 2014

Post a Comment

 
Top