Hivi inakuwaje pale unapokwenda kwenye ATM kutoa pesa toka kwenye akaunti yako na badala ya pesa kutoka anachomoza nyoka anayejaribu kukuua kwa sumu yake kali?, hiyo imetokea kweli nchini Hispania.
Mwanaume mmoja wa nchini Hispania alinusurika maisha yake baada ya kunusurika kugongwa na nyoka wakati akitoa pesa toka kwenye ATM.
Mwanaume huyo alienda kwenye mashine ya kutoa pesa ATM iliyopo nje ya benki ya Caja Madrid bank katika mji wa Llodio, kaskazini mwa Hispania.
Katika hali ambayo hakuitegemea, zilichomoza pesa sambamba na nyoka ambaye alijaribu kumgonga kwenye mikono yake. Pamoja na hayo jamaa hakuziacha pesa zake zikining'inia kwenye ATM, alizichukua pesa zake kabla kuwapigia simu polisi kuwajulisha juu ya tukio hilo.
Kwa msaada wa meneja wa benki, polisi walifanikiwa kumtoa nyoka huyo na kumweka kwenye boksi ili waweze kumrudisha porini.
Inavyoonekana ni kwamba nyoka huyo huenda aliingia mwenyewe ndani ya ATM kwakuwa ATM hiyo ipo karibu na kichaka.
Angalia VIDEO ya nyoka huyo kwenye ATM wakati polisi akijaribu kumtoa kwa kutumia fimbo.
kama kifaa chako hakina Uwezo bonyeza Hapa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- kama siku yako haijafika ni haijafika tu… tazama hizi dakika 9 uone watu wanavyokoswakoswa18 Dec 20150
Ni kumuomba Mungu tu siku zote na kama hajapanga hiyo siku iwe ya mwisho kwako, hata iweje haitak...Read more ?
- Leo nimekuletea hii utazame barabara 10 hatari kwenye hii dunia! kosa moja tu la dereva….14 Jul 20150
Kuna sehemu za hatari sana duniani ambazo unaambiwa ukifanya kosa moja tu unajiweka k...Read more ?
- AJABU:Mwanaume Apandikiziwa Uso wa Mtu Mwingine Baada ya Uso wake Kuaribika na Kuwekewa Sura ya Mtu aliyekufa31 May 20150
Picha ikimwonyesha Norris kabla hajapata ajali, alivyopata ajali na baada ya kuwekewa uso mwingin...Read more ?
- Maajabu: Kila mtu na starehe yake…lakini ya bibi huyu ni kula mchanga kila siku!!15 May 20150
Kibonajoro.com iliwahi kuandika stori ya mama mmoja Evelyne kutoka Missouri, Mare...Read more ?
- Maajabu! Mwanadada Ajifungua 'NAZI' badala ya Mtoto,Ushirikina watajwa30 Apr 20150
Maajabu! Msichana aliyefahamika kwa jina la Dora mkazi wa Magomeni Bagamoyo mkoani Pwani, hivi k...Read more ?
- Ajabu na kweli Ng'ombe Awala Kondoo Kenya, Akataa Kula Majani...(Video)!!24 Apr 20150
Mkulima mmoja nchi Kenya anasema kuwa mmoja wa ng'ombe wake amesusia lishe yake ya kawaida na...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment