Leo Novemba 21, Diamond amesikika kwenye show ya XXL
ambapo amezungumzia mambo mengi, baadhi ya yale aliyoyazungumzia ni
pamoja na story zilizoenea mitandaoni kwamba mahusiano ya msanii huyo na
Wema yameisha pamoja na story ambayo imetokana na kuenea kwa picha
mitandaoni za msanii huyo na Zari the Boss Lady kutoka Uganda.
Hii ni sehemu ya mahojiano aliyofanya Diamond kwenye XXL:
Adam Mchomvu :”…Nataka
kujua ile vibe ya Fiesta that day, story zilikuja ooh Diamond
kazomewa.. kazomewa kazomewa..na vitu kama vile, sijapata chance ya
kukusikia wewe una kipi cha kuzungumzia kuhusiana na that situation..?“
Diamond :- “…
Siku zile kwangu ilikuwa kama mchezo, unajua muziki ushakuwa kama sio
fani tena, ushakuwa kama siasa.. So, lazima uichukulie hivyo wewe
mwenyewe kama msanii ujue una control vipi kwa sababu sio mara ya kwanza
vitu kama hivyo vishatokea Maisha.. Maisha yalitupwa mpaka na mayai
viza kabisa.. Ni vitu ambavyo vikitokea naonaga kama ni kawaida…“
B 12 :-“…Kwa hiyo ukweli uko wapi kati yako wewe na Wema Sepetu?...”
Diamond :- “…Kuna
vitu vitu fulani nadhani kuvizungumza sio vizuri… Lakini ikifikia
kuvizungumzia vinazungumziwa… Uzuri wa mahusiano yetu ni kwamba kila mtu
anafahamu… Haijafikia kuweka wazi ndio maana ninapoulizwa inakuwa ni
swali gumu kulijibu.. “
B 12 :- “.. Ni gumu kwa upande wako lakini yeye yuko tayari kuzungumza kwamba it’s over kati yangu mi’ na Diamond…“
Diamond :- “… Sijui…“
B 12 :- “...Hii
ngoma kama umemzungumzia yeye direct hivi… watu wamekuza akili zao
zikaenda mbali zaidi kimawazo lakini, kwamba inawezekana ile singo
umemwimbia yeye hivi kwamba bado unamzimia japokuwa bado kama kakutosa
hivi…“
Diamond : “.. Waswahili
wanasema ‘A’ na ‘B’ yote majibu, halafu ukisikiliza ile nyimbo kama
kweli mtu mwenye ufahamu wako, kweli kabisa hauwezi kuwa na maswali
mengi …“
Kuhusiana na mahusiano yake na Zari the Boss Lady, Diamond amejibu hivi:
Diamond :- “..
Zari ni rafiki yangu tu, alipokuja hapa mimi ndio nilikuwa mwenyeji
wake Tanzania na kama mimi ndiyo mwenyeji sikutaka kuleta roho za
kibaguzi, unajua hata alipokuja Davido pia ilibidi awe na mimi karibu
ili hata kesho na kesho kutwa mimi nikiwa Nigeria basi Davido anipokee
hivyo hivyo…“
Iko hapa full Interview ya Diamond kwenye XXL, unaweza kuisikiliza kwa kubonyeza play.
Credit Millardayo
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Diamond kuwania tuzo 5 za Afrima 2016, Alikiba na Yamoto Band moja08 Sep 20160
Diamond Platnumz ametajwa kuwania vipengele vitano kwenye tuzo za mwaka huu za Afrima. Vipeng...Read more ?
- Ujumbe wa Diamond kwa bintiye Wazua Gumzo......Kamwambia "Ukikua chonde mama ukitunze wasikile sana"23 Jul 20160
Diamond Platnumz si mgeni kwenye jumbe tata kwenye mitandao ya kijamii. Lakini ujumbe wake mpya...Read more ?
- Bifu Kali Kati ya Diamond na Clouds Media23 May 20160
Ni dhahiri sasa msanii wa kimataifa Diamond na brand kubwa ya radio na tv Clouds Fm, bifu la hadh...Read more ?
- Afande Sele Aungana Na Mbunge Joseph Msukuma Kuitaka Serikali Ihalalishe Matumizi Ya Bhangi02 Feb 20160
Msanii mkongwe wa hip hop nchini, Afande Sele amefunguka na kusema serikali ihalalishe matumiz...Read more ?
- Gari Jipya Analomiliki Masanja Mkandamizaji.10 Jan 20160
Msanii wa Vichekesho Anawakilisha kundi la Orijino Komedi anayejulikana kama Masanja Mkand...Read more ?
- Zari The Lady Boss Awakosha Mashabiki wa Penzi lake na Diamond Kwa Picha Hizi09 Jan 20160
Zari the Boss Lady ‘Mama Tiffah’ amewakosha mashabiki wa penzi lake na Diamond ‘Baba Tiffah’ baada...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment