Stori: Erick Evarist na Musa Mateja
MIEZI michache kufuatia tamko la serikali kuzuia ngoma zinazokesha maarafu kama Kanga Moko kwa kukiuka maadili, imebainika kuwa ngoma hizo zinaendelea kufanya mambo kama kawa kana kwamba hazijakatazwa, Ijumaa limeshuhudia.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili juzikati umebaini kuwa ngoma hizo ambazo wanawake hucheza wakiwa ndani ya kanga moja, zinaendelea kufanyika kwa siri katika viunga mbalimbali vya Jiji la Dar es Salaam.Chanzo makini kimevujisha habari kuwa, wahusika wamekuwa wakipashana habari kupitia kwenye mitandao ya kijamii kisha kukutana katika maeneo tulivu hasa kwenye fukwe na kufanya yao.
“Siku hizi wanatangaziana kwenye mitandao ya kijamii kisha mashabiki na wadau wakubwa wa ngoma hizo wanakwenda kuwashuhudia,” kilisema chanzo.Kuonesha kwamba kipo ‘serious’, chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kwa kunyetisha siku ambayo ngoma hizo zilifanyika katika ufukwe mmoja uliopo Mikocheni jijini Dar.
“Jumamosi hii (iliyopita) watafanya mambo yao katika ufukwe wa...(anautaja jina) uliopo maeneo ya Mikocheni, kama mtaweza fikeni muone jinsi usiku unavyotumika vibaya na ngoma hiyo,” kilisema chanzo hicho.
Siku ya tukio, mapaparazi wetu walitinga katika ufukwe huo na kujionea wadada watatu wakionesha ufundi wa kucheza ngoma hiyo wakiwa wamevalia kanga moja kama kawaida yao.Mara baada ya mapaparazi wetu kunasa picha kadhaa, walijaribu kuwauliza wadada hao kwa nini wanakaidi agizo la serikali, lakini hawakuwa tayari kuzungumza lolote.
Mapema mwaka huu, Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), lilipiga marufuku ngoma hizo kwa kuonekana hazina maadili na si utamaduni wa Mtanzania.
Chanzo Global
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- VIDEO: Mama Wema Aeleza Beef yake na Man Fongo Kisa……..09 Sep 20160
NI Mama Wema Sepetu ambae ameingia kwenye headlines mitandaoni baada ya kutofautiana na mkali wa ...Read more ?
- Busu la Nelly Kamwelu shavuni kwa Diamond akiwa na Wizkid lawatoa povu mashabiki (Video)25 Aug 20160
Haipiti wiki bila Diamond kuwatoa povu mashabiki, hata kama alichokifanya si kwamba alidhamiria...Read more ?
- Picha za Masanja na Mke wake Zazua Maswali Kwa Mashabiki wake..Wadai Mke wa Mchungaji Apaswi Kuvaa Hivyo19 Aug 20160
Baada ya Harusi ya Mchekeshaji Masanja na Mkewe iliyofungwa Jumapili iliyopita wawili hao wameon...Read more ?
- AUDIO: Kitu Diamond kasema kuhusu yeye kuwa mapenzini na Hamisa Mobetto03 Aug 20160
Ukaribu wako kwenye mitandao ya kijamii siku za karibuni unaweza kuwa ulikukutanisha na stori...Read more ?
- Shamsa Ford Amuweka Wazi Mpenzi wake Mpya03 Aug 20160
Msanii wa filamu nchini Shamsa Ford amefunguka na kusema kuwa baada ya kuachana na mpenzi wake wa...Read more ?
- Madai: Flora Amwangukia Mbasha30 Jul 20160
Habari ya mjini ni Mwimba Injili Bongo, Flora Mbasha kudaiwa kumwangukia mumewe waliyetengana, Em...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment