STAA wa filamu Bongo, Chuchu Hans amedhihirisha kwamba
ana mahaba niue kwa mpenzi wake, Vincent Kigosi ‘Ray’ kwa kulinadi jina
lake hadharani kwa kuvaa t-shirt iliyoandikwa; ‘Ray Kigosi’.Tukio hilo
lilichukua nafasi wikiendi iliyopita kwenye Tamasha la Usiku wa
Matumaini lililofanyika katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar ambapo
mwanadada huyo aliambatana na mashosti zake kushuhudia burudani tofauti
ikiwemo mechi ya timu ya Bongo Fleva na Movies anayoichezea mpenzi wake.Chuchu
alivaa t-shirt ya njano ambayo mgongoni ilikuwa imeandikwa Ray Kigosi
kitu ambacho hakuwahi kukifanya kabla.
Sioni tatizo kujinadi hadharani, atakayemaindi shauri yake, nafanya kitu roho inapenda bwana sijali maneno ya watu hata kidogo
alifunguka Chuchu.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:-
0712483331.
Like ukurasa wetu wa facebook ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment