Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Anawasili: Mario Balotelli aliyepigwa picha hii mwaka jana, anatua Liverpool leo kukamilisha usajili wake

MSHAMBULIAJI Mario Balotelli alitarajiwa kuwasili England leo mchana kwa ajili ya kufikia makubaliano ya kujiunga na Liverpool baada ya klabu hiyo kufikia makubaliano na wawakilishi wake.

Mpachika mabao huyo wa zamani wa Manchester City yuko karibu kusaini kikosi cha Brendan Rodgers na amekwenda huko kukamilisha dili hilo mara moja. 

Baada ya kuwasili, Balotelli alitarajiwa kwenda kufanyiwa vipimo katika hospitali ya klabu hiyo, Spire Liverpool kabla ya kwenda kufanyiwa vipimo zaidi vya afya katika viwanja vya Melwood vinavyotumika kwa mazoezi na klabu hiyo.
Pamoja na hayo, mshambuliaji huyo wa Italia hataweza kuichezea Liverpool dhidi ya klabu yake ya zamani, Manchester City Jumatatu usiku, katokana na muda wa usajili kwa leo kupita.
Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyeza hapa



Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top