Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
MUSTAKABALI wa Mohamed Salah katika klabu ya Chelsea upo shakani, baada ya kutakiwa kurejea nyumbani kwao, Msiri kuchukua mafunzo ya jeshi.

Salah, aliyehamia Stamford Bridge kutoka Basle ya Uswisi Januari mwaka huu, ameruhusiwa kuishi England kwa kigezo cha kushiriki masomo. Pamoja na hayo, usajili wake umesitishwa na Wizara ya Elimu ya Juu Misri, tovuti ya soika ya www.kingfut.com imesema, maana yake mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 anaweza kurudi nchini mwao.
Jeshini kwanza; Mo Salah anatakiwa kurudi nyumbani kupata mafunzo ya Jeshi Ikiwa Salah, aliyeichezea Chelsea mchezo wa kirafiki dhidi ya AFC Wimbledon jana atatakiwa kurejea nyumbani, hataruhusiwa kuondoka tena Misri hadi akamilishe mafunzo ya kijeshi, yanayochukua mwaka mmoja hadi mitatu. "Salah ameelesea namna alivyoshitushwa juu ya uamuzi huu," amesema Mkurugenzi wa timu ya taifa ya Misri, Ahmed Hassan.
"Ameniambia anajaribu kuiwakilisha Misri katika njia nzuri zinazowezekana. Na haya ndiyo matokeo yake kutoka kwa nchi yake?' Kikao kinatarajiwa kufanyika baina ya FA ya Misri, benchi la ufundi la timu ya taifa na Waziri wa Elimu ya Juu, kutafuta suluhisho.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
 
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top