Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Shirika la kutetea haki za wanyama la Afrika Kusini limeanza uchunguzi kuhusiana na kifo cha twiga baada ya kuumia wakati akisafirishwa kwenye gari. Watu walioshuhudia tukio hilo wanasema twiga mmoja kati ya wawili waliokuwa kwenye lori, aligonga kichwa chake katika barabara moja mjini Johannesburg. Gari hilo baadaye liliharibika na kulazimika kusubiri kwa saakadhaa kabla ya kutengenezwa. 
 
Wanyama wote wawili walipelekwa kwa daktari wa wanyama, lakini shirika la kutetea haki za wanyama la NSPCA limesema twiga mmoja alikufa. Tukio hilo limeleta mjadala mkubwa kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter. Meneja wa NSCPA Rick Allen amethibitisha kuwa twiga huyo alipata majeraha ya kichwani lakini amesema uchunguzi ni muhimu ufanyike kutafuta sababu hasa ya kifo hicho.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331

kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top