SHIRIKA
la Ugavi wa Umeme (Tanesco) Mkoa Pwani, limefanikiwa kumkamata Jeams
Mkelembwa ambaye anadaiwa kuwatapeli wananchi kwa kujifanya mtumishi wa
shirika hilo.
Akizungumza kuhusu
sakata hilo jana, Ofisa Usalama wa Tanesco Pwani, Henry Byarugaba,
alisema kwamba tukio la kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo lilitokea juzi
wilayani Kisarawe wakati alipokuwa akitaka kumtapeli mteja mmoja wa
umeme.
Byarugaba
alisema mtuhumiwa huyo amekuwa akitumia njia mbalimbali ikiwemo kutumia
majina ya viongozi, pamoja na kudai yeye ndiye Meneja wa Tanesco Mkoa
wa Pwani, kitu ambacho si cha kweli.
“Ndugu
mwandishi, katika siku za hivi karibuni tulikuwa na zoezi maalumu la
kukagua miundombinu yetu ya umeme katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa
Pwani, lakini tulipata fununu kuna baadhi ya watu wanajifanya wao ni
wafanyakazi wa shirika letu na kuwatapeli wateja wetu, hali ambayo
inasababisha lawama nyingi kutolewa kwetu…
“Huyu
jamaa tuliyemkamata ni hatari sana, kwani ameshafanya matukio mengi ya
utapeli kwa wananchi, maana anatumia vyeo vya watu mbalimbali ikiwemo
kujifanya yeye ni ofisa wa Tanesco, mara mtumishi kutoka wizara fulani
mara Takukuru, yaani ni balaa tupu, kumbe ni kishoka maarufu sana na
mimi nitahakikisha anachukuliwa hatua kali za kisheria ili iwe
fundisho,” alisema Byarugaba.
Alisema
mtuhumiwa huyo kwa sasa anashikiliwa na polisi Kisarawe na kuwaomba
wateja wote ambao wametapeliwa na mtu huyo waende kwa ajili ya
kumtambua.
Byarugaba
aliongeza kuwa tapeli huyo alishafanya matukio ya kuwaibia watu katika
maeneo mbalimbali ikiwemo Majohe, Pugu, Chanika na mengineyo.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment