
Mpiganaji wa kundi la waasi wa Tuareg nchini Mali
Waasi nchini Mali wamekubali kusitisha vita siku mbili baada ya kuvishinda vikosi vya serikali katika mji wa kazkazini wa kidal.
Takriban wanajeshi 20 wa Mali waliuawa baada ya jaribio la kutaka kuuteka mji huo kutoka kwa waasi hao kufeli siku ya jumatano.
Waasi hao wameiambia BBC kwamba wanadhibiti eneo lote la kazkazini mashariki mwa Mali na sasa wanaelekea katika mji wa Gao.
Serikali imewashtumu waasi hao kwa kuungwa mkono na wapiganaji wa kundi la Al Qaeda.
Chanzo bbcswahili
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment