Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Screen Shot 2014-05-29 at 10.01.00 AM
Kwenye zile stori za maisha ya mastaa wa soka Ulaya wiki hii, hii nayo ni moja ya stori kubwa ambapo ilisambaa kupitia vyombo mbalimbali vya habari likiwemo gazeti la Daily Mail lililoripoti kuhusu gari la mchezaji huyu wa Manchester City kubebwa juujuu na Polisi kwa makosa ya kupaki ovyo.

Ripoti ilitoka kwamba staa huyu ambae atalitazamia kombe la dunia nyumbani kwa sababu hajapangwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ufaransa amepata habari nyingine isiyo nzuri baada ya gari lake kubebwa juujuu kutokana na makosa ya parking, yani liliegeshwa kimakosa.
Screen Shot 2014-05-29 at 10.02.17 AM
Pamoja na kwamba ripoti ilisema Samir atalazimika kwenda kulichukua hili gari yeye mwenyewe kwenye mamlaka husika, staa huyu alikanusha kuwa mmiliki wa hilo gari na kusisitiza kwa kuliambia gazeti ‘Daily mail fanyeni utafiti, hilo halijawahi kuwa gari langu’ 
Screen Shot 2014-05-29 at 10.01.12 AM

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top