Ghasia hizo
zilianza kufuatia kifo cha mwanamume mwenye umri wa miaka 26, Douglas
Rafael da Silva, mchezaji densi wa kulipwa. Kulingana na familia yake
mwili wake ulipatikana ukiwa umejaa vidonda na waliwalaumu maafisa wa
polisi kwa kumpiga hadi kufa baada ya kumshuku kuwa mwanachama wa genge
moja linalouza madawa ya kulevya.
Watu
walikusanyika katika lango la kuingia katika makaazi hayo ya mabanda
alikopatikana mtu huyo akiwa ameauwa na wakataka kujua kutoka kwa
maafisa wa polisi sababu za kuuliwa kwake. Polisi kadhaa wa kijeshi
wenye silaha wako mahali hapo kufuatia habari kuwa kituo cha polisi
kilichoko mahali hapo kimevamiwa.
Pavaozinho
ni mojawapo ya makaazi ya mabanda ambayo Serikali Kuu ya Brazil
imejaribu kuwatimua magenge ya walangunzi wa madawa ya kulevya wenye
silaha kutoka kwa jamii na kueneza amani na mmalaka ya polisi. Polisi
wamekiri katika mahojiano na BBC kuwa wameshindwa kuthibiti usalama
katika makaazi ya mabanda katika mji mkuu wa Rio de Jenairo, muda mfupi
tu wakati ambapo wageni wengi wanatarajiwa nchini humo, kukiwemo maelfu
wanaotarajiwa nchini kwa sababu ya Kombe la Dunia.
Chanzo - BBC Swahili
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment