Story hii ya kusikitisha inatoka Kenya ambapo jamaa mmoja Daniel Imonje, alimpiga mke wake kwa shoka mpaka kufariki, majirani walioshuhudia wakisema eti kisa ilikuwa ni kitendo cha mke wake huyo kutomuandalia mume wake nyama ya kuku siku ya Christmas, badala yake akaandaa rosti ya nyama ya ng’ombe.
Ni wengi waliolaani kitendo hicho kilichotokea Kijiji cha Shanderema, Kenya na mashuhuda wamesema Daniel alifanya unyama huo akiwa amelewa.
Mtuhumiwa anashikiliwa katika kituo cha Polisi cha Kakamega baada ya kufanya mauaji hayo kwa ajili ya uchunguzi.
Credit Millard ayo
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro






Post a Comment
Post a Comment