Dereva wa
Bodaboda aliyejulikana kwa jina la Musa Wambari, 25, mkazi wa Kitunda,
jijini Dar es Salaam amekutwa amenyongwa na maiti yake kutupwa katika
Uwanja wa Shule ya Abdu Juma huko Kivule.
Tukio hilo la kuhuzunisha lilitokea Februari 9, mwaka huu saa 4 usiku baada ya marehemu kukodiwa na watu wawili.
Imedaiwa
na madereva bodaboda waliokuwa wakiegesha pikipiki zao eneo la Matembele
na marehemu kuwa, siku ya tukio wakiwa eneo lao la kazi alifika kijana
anayedaiwa kujihusisha na uhalifu aitwaye Jose akiwa na mwenzake
aliyevaa suti.
Mmoja wa
madereva hao aliyeomba hifadhi ya jina lake aliongeza kuwa, Jose na
rafiki yake walitaka kukodi pikipiki lakini kwa vile walikuwa
wakimfahamu kwamba alikuwa muhalifu walikataa ndipo wakaondoka.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro






Post a Comment
Post a Comment