March 16, 2025 12:10:07 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA jana alitembelea shule ya Nanja iliyoungua moto hivi karibuni mkoani Arusha.

Akiambatana na viongozi wengine katika jimbo la Monduli Lowassa aliwataka viongozi kuhakikisha shule za bweni zinajengwa vizuri na kuwekewa mifumo ya kujikinga na ajali za moto kama ambavyo sasa shule tano kwa kipindi kifupi zimeungua moto mkoani Arusha na chanzo kikiwa hakijulikani.

“Napenda kuwakumbusha wakuu wa shule na viongozi kwamba ni muhimu shule zote za mabweni ziwezeshwe na zijengwe vizuri huku zikichukuliwa tahadhari zote za kujikinga na ajali kama hizi, pia nitaungana na uongozi wa jimbo la Monduli pamoja na wadau mbalimbali kuhakikisha shule hii inarekebishwa na watoto wanarejea katika mabweni” Alisema Lowassa.

Aidha Lowassa alitumia nafasi hiyo kuwaasa wanafunzi kusoma kwa bidii kwani elimu ndiyo mkombozi wa maisha yao.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
19 Aug 2016

Post a Comment

 
Top