Diwani wa kata ya Kimwani iliyoko Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera, Silvester Miga (CUF) amepoteza maisha baada ya kuvamiwa na kukatwa na mapanga nyumbani kwake, usiku wa kuamkia jana.
Kamanda wa Polisi Mkoani Kagera, Augustine Ollomi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa marehemu alipoteza maisha majira ya saa saba usiku akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Kagondo.
Imeelezwa kuwa Miga alivamiwa nyumbani kwake akiwa anaangalia taarifa ya habari kwenye runinga ambapo watu hao walimvamia na kutekeleza tukio hilo la kikatili.
Kamanda Ollomi alisema kuwa Jeshi la Polisi mkoani humo limeendesha msako mkali na kuwakamata watu wawili wanaotuhumiwa kuhusika na tukio hilo.
Aliwataja watu hao kuwa ni Aderarid Antony mwenye umri wa miaka 42 na Shiranga Gonzari mwenye umri wa miaka 22.
Baadhi ya wakazi wa kata Kimwani waliwaambia waandishi wa habari kuwa mazingira ya kuuawa kwa diwani wao ni ya kisiasa zaidi.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 12011 Sep 20160
Tetemeko la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nc...Read more ?
- Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.09 Sep 20160
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao uliku...Read more ?
- Polisi Washuhudia Majambazi Yakitwangana Risasi.......Zakamatwa Shehena za Silaha na Vifaa vya Uhalifu06 Sep 20160
WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wa kutumia silaha, ambao wamehusika kufanya matukio ...Read more ?
- Askari Magereza Atiwa Mbaroni Kwa Kuingia Wodini Akiwa Amelewa na Kisha Kuanza Kufyatua Risasi28 Aug 20160
POLISI mkoani Rukwa inamshikilia askari Magereza, Cleophas Chapaulinge kwa kosa la kulewa na k...Read more ?
- Polisi Mwingine Auawa Kwenye Mapambano Makali na Majambazi Huko Mkuranga27 Aug 20160
Ilikuwa ni kama filamu ya askari na maadui wakati askari wa Jeshi la Polisi walipopambana na wat...Read more ?
- RC Makonda: Polisi Mkikuta Mtu Yeyote Msituni Pigeni bila Huruma.......Haki za binadamu Wakiwauliza Waambieni waje Kwangu26 Aug 20160
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameliagiza Jeshi la Polisi kuwagonga na kuwapiga wah...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment