Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue ameagiza na kusisitiza ofisi zote Umma kusimamia na kuhakikisha kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu kila watumishi awe na kitambulisho (beji) kinachoonesha jina lake.
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Balozi Sefue alisema hatua hiyo ya watumishi wa umma kuvaa beji zenye majina kila wakati wanapotekeleza majukumu yao itasaidia wananchi kuwatambua kwa majina watumishi wanaowahudumia na kuwasaidia kulingana na mahitaji yao kwenye ofisi hizo.
Ili kutekeleza azma ya kuwahudumia wananchi, Balozi Sefue alisema kuwa kuanzia sasa watumishi wote wa umma wavae beji zenye majina yao iwe rahisi kwa mwananchi kumtambua anayemhudumia na hivyo kumsifu mtumishi wa umma anayewahudumia kwa weledi, uaminifu na kwa wakati na kumtolea taarifa yule anayefanya mambo ya hovyo.
Zaidi ya hayo, Balozi Sefue amewahimiza viongozi na watumishi wote katika Utumishi wa Umma kubadilika kwa dhati kwenye utendaji na uadilifu wao na kuwahudumia wananchi kwa haki, weledi, uadilifu na heshima.
“Rais na sisi wote tunaomsaidia hatuoni raha kuchukua hatua dhidi ya viongozi na watumishi wengine, tungependa kila mtu mwenyewe ajirekebishe na kutomfikisha Rais mahali ambapo inabidi amchukulie hatua” alisema Sefue.
Mambo muhimu yanayopaswa kuzingatiwa ni pamoja na kila kiongozi na mamlaka ya nidhamu isipate kigugumizi kusimamia utendaji na maadili ya kazi ili kuchukua hatua za nidhamu, lakini afanye hivyo kwa kuzingatia kwa ukamilifu sheria, kanuni na taratibu katika Utumishi wa Umma.
Balozi Sefue amewahimza viongozi na watumishi wa umma kuwahudumia wananchi kwa haki, weledi, uadilifu na heshima ambapo kila ofisi ya Serikali inapaswa kuwa na dawati la kusikiliza shida za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Kwa upande wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya wote nchini wametakiwa kujenga uwezo wa kushughulikia shida za wananchi kwa ukamilifu na kwa wakati.
“Kwa muundo wa Serikali yetu hakuna sababu kwa mwananchi kufunga safari mpaka Ikulu Dar es Salaam kwa kuamini kuwa ni Rais tu ndiye anayeweza kumaliza matatizo yake, maana wawakilishi wa Rais wako kila pembe ya nchi yetu, ikibidi wananchi wafike Ikulu inamaana hao wawakilishi wa Rais hawakutimiza wajibu wao” aliongeza Balozi Sefue.
Aidha, Balozi Sefue alisema kuwa ofisi zote za Serikali zinatakiwa kuwa na dawati la kupokea maoni ya wananchi kuhusu huduma inayotolewa kwenye ofisi hizo na kushughulikia haraka maeneo yote ambayo wananchi wataonesha kutoridhika na huduma inayotolewa.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Jamaa Aliyejitosa Zoo Aliwe na Simba Laivu Alikuwa Anadai Mwisho wa Dunia Umefika...23 May 20160
Inasikitisha kwakweli, ameokolewa.... na simba walioanza kumla waliuwawa. aliingia kwenye jumba ...Read more ?
- Watumishi HEWA Waziponza Benki.......Benki za Dar es Salaam Zalimwa Barua Kurejesha Mamilioni ya Shilingi23 May 20160
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametoa siku 21 kwa benki zilizokuwa zikitumika kuwek...Read more ?
- Waziri Nchemba Afanya Ziara Ya Kushtukiza Saa Saba Usiku Machinjio Ya Ukonga Mazizi Na Kufukuza Viongozi Wote Wa Machinjio12 Feb 20160
Waziri wa Kilimo na Mifugo Mwigulu Nchemba amefanya ziara ya Kushtukiza saa saba usiku...Read more ?
- Askofu Gwajima, Sheikh Wa Mkoa Dar Wakwama Kumjulia Hali Mufti12 Feb 20160
Jopo la Madaktari wanaomtibu Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir wamezuia ...Read more ?
- Siku 100 za Rais Magufuli: Hospitali Ya Muhimbili Yang'aa, Mapato Yapaa na Upatikanaji wa Dawa Waongezeka Kwa Asilimi 9611 Feb 20160
HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili (MNH) iliyopo jijini Dar es Salaam imesema ndani ya siku 100 z...Read more ?
- Lowassa Atakiwa Kuvisaidia Vyombo Vya Dola Kukabiliana na Tishio La Kundi la al Qaeda Kuingia Nchini10 Feb 20160
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed Aboud Mohamed amemtaka Wa...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment