OFISA wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) mkoani Dodoma, Emmanuel Meta (37) ameuawa kufuatia kupigwa na kukatwa mapanga cha watu ambao mpaka sasa hawajafahamika.
Hata hivyo Jeshi la Polisi linamshikilia mtu mmoja kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo.
Tukio hilo lilitokea Januari 20, mwaka huu majira ya saa 6:15 usiku katika eneo la Area C manispaa ya Dodoma.
Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), David Mnyambuga, Ofisa huyo wa PCCB alifariki dunia wakati anapatiwa matibabu baada ya kupigwa na watu ambao hakuwafahamu.
Alisema mtoa taarifa wa awali wa tukio hilo, Athuman Mtengwa ambaye pia ni mfanyakazi PCCB, mkazi wa Area “D” alieleza kuwa, Januari 20, saa 6:15 usiku akiwa nyumbani kwake alipigiwa simu na Emmanuel (marehemu) ambaye ni mfanyakazi mwenzake pia ni rafiki yake wa karibu.
Alisema Meta alimweleza kuwa anaomba msaada wa kupelekwa hospitali kutibiwa kwa kuwa amepigwa na watu wasiofahamika wakati akirudi nyumbani kwake akitokea baa ya Rose Garden iliyopo Area “C” jirani na nyumbani kwake kwa matembezi.
Baada ya Mtengwa kufika alipiga honi ndipo Meta alitoka nje na kufunga mlango na geti kwa kufuli na kuingia katika gari kuelekea Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na wakiwa njiani hali yake ilibadilika na kukosa nguvu na kushindwa kujimudu kwa lolote.
Alisema wakati akiendelea kupatiwa matibabu Hospitali ya Mkoa wa Dodoma alifariki dunia.
Kaimu Kamanda alisema uchunguzi wa mwili wa marehemu umefanyika ambapo amekutwa na jeraha kichwani linalovuja damu, alitokwa na damu puani na masikioni, uvimbe katika jicho la kulia na michubuko midogo mikononi.
“Mtu mmoja anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano zaidi na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo unaendelea,” alisema Kaimu Kamanda.
Alitoa wito kwa mtu au watu wenye taarifa kuhusiana na tukio hili washirikiane na Jeshi la Polisi kuwafichua watu waliofanya uhalifu huo ili sheria ichukue mkondo wake.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 12011 Sep 20160
Tetemeko la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nc...Read more ?
- Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.09 Sep 20160
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao uliku...Read more ?
- Polisi Washuhudia Majambazi Yakitwangana Risasi.......Zakamatwa Shehena za Silaha na Vifaa vya Uhalifu06 Sep 20160
WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wa kutumia silaha, ambao wamehusika kufanya matukio ...Read more ?
- Askari Magereza Atiwa Mbaroni Kwa Kuingia Wodini Akiwa Amelewa na Kisha Kuanza Kufyatua Risasi28 Aug 20160
POLISI mkoani Rukwa inamshikilia askari Magereza, Cleophas Chapaulinge kwa kosa la kulewa na k...Read more ?
- Polisi Mwingine Auawa Kwenye Mapambano Makali na Majambazi Huko Mkuranga27 Aug 20160
Ilikuwa ni kama filamu ya askari na maadui wakati askari wa Jeshi la Polisi walipopambana na wat...Read more ?
- RC Makonda: Polisi Mkikuta Mtu Yeyote Msituni Pigeni bila Huruma.......Haki za binadamu Wakiwauliza Waambieni waje Kwangu26 Aug 20160
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameliagiza Jeshi la Polisi kuwagonga na kuwapiga wah...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment