Home
»
wema sepetu
» Wema Sepetu Akubali Kushindwa Adai Siasa Bila Kujipanga Utoki... ‘Utakatwa’ tu!
Leo tunaye msanii wa filamu za Kibongo, Wema Sepetu ambaye hivi karibuni alithubutu kugombea ubunge kupitia viti maalum mkoani Singida.
Kwa bahati mbaya kura za msanii huyu hazikutosha. Mwandishi wetu alionana na mwanadada huyo nyumbani kwake Kijitonyama jijini Dar na kumpiga maswali 10 mujarabu. Ungana nami…
Ijumaa: Hongera kwa kujitosa kwenye siasa, nini kilikusukuma kuingia huko?
Wema: Nilikuwa nashauku ya kuwa mheshimiwa, hata baba yangu aliwahi kuniambia naweza hivyo nikajaribu bahati yangu.
wema (8)Ijumaa: Ukiacha marehemu baba yako, nani alikupa sapoti kubwa na ukajiona unaweza?
Wema: Namshukuru mama yangu, alinipa sapoti kubwa nikajiona naweza kwani alinitoa hofu niliyokuwa nayo.
Ijumaa: Unadhani kipi kimekuangusha kwenye uchaguzi ule?
Wema: Uchanga wangu kwenye siasa lakini naamini muda ulikuwa bado.
Ijumaa: Ingawa hukufanikiwa kupata nafasi ya ubunge umejifunza nini kupitia siasa?
Wema: Kwa kweli nimejifunza vitu vingi maana haviendani hata na umri wangu na nimepata ujasiri mkubwa. Kikubwa ukiingia kwenye siasa ujipange sana.
Ijumaa: Je, kwa hatua uliyoifikia unategemea kuendelea na siasa?
Wema: Niache? Siwezi kwani itakuwa kazi yangu, kama gari ndiyo limewaka sasa.
Ijumaa: Najua siasa ni hela hasa kipindi cha kampeni, uliwezaje kumudu gharama zote?
Wema: Ni rahisi sana ukiwa na watu wanaokupenda, walijitokeza watu kunichangia kwa ajili ya kuhakikisha nafanikiwa. Siwezi kuwataja lakini nawashukuru sana.
Ijumaa: Tulipata habari kwamba baada ya kushindwa uliangua kilio, kwa nini?
Wema: Unajua unapoenda kufanya kitu lazima una matumaini japo kuna kushindwa lakini kushinda ndiyo lengo sasa usipofanikisha lazima roho inauma.
Ijumaa: Ulijisikiaje ulipokuta nyomi la watu wakikusubiri kwa ajili ya kukupokea wakati hukuwa umeshinda?
Wema: Niliamini nina watu wengi ambao wananipenda na nilijifunza mengi kupitia ujio wao, pia walinitia moyo wa kuendelea na siasa.
Ijumaa: Kuna madai kuwa baada ya kushindwa una mpango wa kuhamia Ukawa, hilo unalizungumziaje?
Wema: Ninachojua watu wa Ukawa wamenitafuta na ilikuwa tukutane jana (Jumatatu) ila tutakutana Jumatano (juzi), nikijua wanachoniitia ndiyo nitafanya uamuzi.
Ijumaa: Baada ya kuingia kwenye mambo ya siasa tumtegemee Wema wa aina gani?
Wema: Mtarajieni Wema wa tofauti na yule mliyemzoea, mambo ya skendoskendo hayatakuwa na nafasi kwenye maisha yangu.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- VIDEO: Mama Wema Aeleza Beef yake na Man Fongo Kisa……..09 Sep 20160
NI Mama Wema Sepetu ambae ameingia kwenye headlines mitandaoni baada ya kutofautiana na mkali wa ...Read more ?
- Wema Sepetu ampigia magoti Idris Sultan22 Aug 20160
Uhusiano wa Wema Sepetu na Idris Sultan unaanza kutukumbusha ule wa Chris Brown na Karrueche Tr...Read more ?
- Wema Sepetu: Niacheni jamani Nimechoka03 Aug 20160
Wema Sepetu Msanii wa filamu nchini Wema Sepetu ameonesha kuchoka na maneno mbalimbali k...Read more ?
- Idris Sultan Amtundika Mimba Wema Sepetu25 Jan 20160
Mshindi wa Big Brother Afrika, Idris Sultan amepasua jipu kuhusu uhusiano wake na Wema Sepetu...Read more ?
- Kipindupindu Chanyemelea Nyumbani Kwa Wema Sepetu28 Aug 20150
Mrembo Wema Sepetu Taarifa za ugonjwa wa kipindupindu zimebadili mfumo wa maisha ya watu wengi i...Read more ?
- Wema Sepetu na Lowassa ni 'Paka na Chui'......Atoa ONYO Kali Kwa Team Wema11 Aug 20150
Kama unamfatilia Wema Sepetu kwenye mitandao yake ya kijamii jana kupitia mtandao wa Instagram a...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment