BIASHARA
ya ngono imeshamiri mkoani Dodoma wakati huu ambao vikao vya kumpata
mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) vimekwisha kuanza.
Uchunguzi
uliofanywa katika baadhi ya kumbi kama Club Maisha, Club Laazizi na
Matei Lounge, Chako ni Chako, umebaini kuwapo idadi kubwa ya kina dada
wakiwa wamevaa nusu uchi.
Katika
maeneo ya katikati ya mji wa Dodoma zilikuwapo hekaheka za wasichana
wanaojiuza ambao walionekana wakitafuta wateja bila ya wasiwasi wowote
na wengine walisikika wakisema wako kibiashara na siyo kuuza sura.
Eneo
maarufu la Chako ni Chako kuanzia jioni mpaka usiku kucha akina dada
hao wamekuwa wakijazana hadi kwenye taa za kuongozea magari huku
wakitafuta wateja wenye magari.
Baadhi yao ambao hawakutaka kutaja majina yao halisi mmoja wao alisema, ‘’Kaka sema una shilingi ngapi habari ya majina unataka kutupeleka wapi…?
‘’……wewe unaona shimo limetema hapa kila nikigeuka mwanaume na wanatoa ‘mpunga’ nadhani huyu rais ajaye atakuwa na neema.’’
Dada
mwingine ambaye aliyekuwa Dodoma Carnival karibu na Kituo Kikuu cha
Mabasi, alisema ametoka Arusha akiwa na marafiki zake kwa lengo la
kuwafuata wateja wa msimu walioko Dodoma.
Alisema
hadi sasa ana siku tatu akiwa Dodoma na tayari amekusanya zaidi ya
Sh 700,000 huku akiwatumia madalali ambao huwaunganisha kwa wateja
‘wazito’ (wenye fedha) kwa ujira maalum.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- BREAKING NEWS: Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha ametangaza rasmi tarehe ya kurudiwa kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar22 Jan 20160
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha ametangaza rasmi tarehe ya kuru...Read more ?
- Rais Dkt. Magufuli Amteua Jakaya Kikwete Kuwa Mkuu Wa Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam.21 Jan 20160
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Rais Mstaafu wa awamu ...Read more ?
- JANUARY MAKAMBAASHANGAZWA NA HAYA MAGAZETI MATATU KUHUSU LOWASSA02 Sep 20150
Naibu waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba ameonesha kushangazwa na mfa...Read more ?
- Polisi Yakamata Majambazi 38 Yakiwa na silaha Nzito pamoja na Milioni 170......Majambazi hayo yanadaiwa na mafunzo ya Kijeshi01 Sep 20150
Jeshi la Polisi limewakamata watu 38 wanaotuhumiwa kuwa ni majambazi ambao pia wamepatiwa mafun...Read more ?
- Wananchi Wafunga Barabara Baada ya Gari la Polisi Kugonga Wanafunzi wawili31 Aug 20150
Wananchi wa eneo la Misugusugu Wilayani Kibaha Mkoani Pwani hii leo wamefunga barabara baada ya...Read more ?
- Hali Tete Bunda, Viongozi CHADEMA Wajiuzulu...Kisa Ester Bulaya22 Aug 20150
SIKU chache baada ya mgombea ubunge wa Jimbo la Bunda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maend...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment