March 16, 2025 04:43:37 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Kikao cha Bunge kilianza kama kawaida leo July 02 2015, baada ya kipindi cha maswali na majibu yaliyoulizwa kwa Mawaziri, Mbunge John Mnyika akaomba mwongozo.

“Tumekabidhiwa orodha ya shughuli za leo.. kimsingi imekiuka kanuni, uamuzi wa kuileta hii miswada mitatu kwa pamoja kama hati ya dharura umekiuka kabisa msingi wa makubaliano ya kwenye Semina ambapo Wabunge kwa kauli moja tulikataa Miswada hii isiletwe kwa hati ya dharura“


“Naomba Mwongozo, hili jambo linahitaji majibu sasa” >>> Mbunge John Mnyika.

Spika Makinda akaanza kutoa ufafanuzi kuhusu hiyo ishu >>> “Toa kwanza maneno ya kuniamrisha mimi cha kufanya… Hakuna mtu anayeweza kuniamrisha” >>> Anne Makinda.

Spika akaendelea >>> “Tumefanya mara nyingi sana wala sio leo tu, hakuna kanuni iliyovunjwa na sio mara ya kwanza kujadili kitu kinachofanana kwa pamoja”>>> Spika Anne Makinda.

Hakukuwa na suluhu ya hilo, Wabunge wa Upinzani wakagomea Mjadala huo kuendelea ikabidi Kikao cha Bunge kiahirishwe saa nne asubuhi. Angalia Video Hapa: 

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
03 Jul 2015

Post a Comment

 
Top