JESHI la Polisi mkoani Kilimanjaro linamshikilia Dainees Fredrick (30), mkazi wa Kambi ya Raha, wilayani Hai, kwa tuhuma za kumuua mtoto wake mchanga muda mfupi baada ya kumzaa kwa kumtumbukiza chooni.
Inadaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alifanya kitendo hicho siku moja baada ya kujifungua ambapo alimfunga mtoto huyo wa kiume kwenye kanga na kumweka kwenye mfuko wa plastiki kisha kumtumbukiza chooni.
Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Fulgence Ngonyani, katika taarifa yake alisema tukio hilo lilitokea Juni 10, saa tatu usiku, Mtaa wa Kambi ya Raha, ambapo waliofanikisha kukamatwa kwake ni majirani anaoishi nao.
Alisema Rose Komely alisikia sauti ya kichanga kikilia ndani ya choo baada ya kwenda kujisaidia, ndipo alipowaeleza wapangaji wengine na kwenda chumbani kwa mtuhumiwa huyo na kumkuta akiwa amekaa huku akiwa hana ujauzito analalamika maumivu ya tumbo.
Ngonyani alisema kuwa mtoa taarifa alimuacha mtuhumiwa akiwa na mwenzake kisha kutoa taarifa kwa balozi Editha John ambaye alitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi.
Hata hivyo, licha ya Jeshi la Polisi kufanikiwa kufika nyumbani kwa mtuhumiwa huyo na kumtoa mtoto katika choo alichokuwa ametupwa tayari mtoto alikuwa amekufa.
Mtuhumiwa wa tukio hilo la mauaji ya kichanga anashikiliwa na Polisi na kwa sasa anaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Hai, huku akiwa chini ya ulinzi akisubiri sheria kuchukua mkondo wake.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 12011 Sep 20160
Tetemeko la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nc...Read more ?
- Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.09 Sep 20160
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao uliku...Read more ?
- Polisi Washuhudia Majambazi Yakitwangana Risasi.......Zakamatwa Shehena za Silaha na Vifaa vya Uhalifu06 Sep 20160
WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wa kutumia silaha, ambao wamehusika kufanya matukio ...Read more ?
- Askari Magereza Atiwa Mbaroni Kwa Kuingia Wodini Akiwa Amelewa na Kisha Kuanza Kufyatua Risasi28 Aug 20160
POLISI mkoani Rukwa inamshikilia askari Magereza, Cleophas Chapaulinge kwa kosa la kulewa na k...Read more ?
- Polisi Mwingine Auawa Kwenye Mapambano Makali na Majambazi Huko Mkuranga27 Aug 20160
Ilikuwa ni kama filamu ya askari na maadui wakati askari wa Jeshi la Polisi walipopambana na wat...Read more ?
- RC Makonda: Polisi Mkikuta Mtu Yeyote Msituni Pigeni bila Huruma.......Haki za binadamu Wakiwauliza Waambieni waje Kwangu26 Aug 20160
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameliagiza Jeshi la Polisi kuwagonga na kuwapiga wah...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment