Home
»
Matukio
» Hiki ndio kilichonifikia kuhusu Makongoro Nyerere kuhusishwa na ajali iliyotokea Kigoma
MSAFARA wa Makongoro Nyerere, mtoto wa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, umepata ajali wakati mwanasiasa huyo akiwa katika harakati za kutimiza masharti ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya kutafuta wadhamini ili aweze kuwania nafasi ya urais.
Ajali hiyo iliyojeruhi watu watano waliokuwa kwenye msafara huo, ilitokea jana katika eneo la Tekniko, Wilaya ya Kasulu, mkoani Kigoma baada ya gari aina ya Land Cruiser lenye namba T 188 BXG walilokuwamo kupinduka.
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ferdinand Mtui, alisema ilitokea saa 10:30 asubuhi wakati msafara huo ukiongozwa na Makongoro ukielekea Kigoma mjini.
Kamishna Mtui aliwataja waliojeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili ikiwamo kichwani na mabegani kuwa ni dereva wa gari hilo Julius Kambarage, ambaye ni mtoto wa Makongoro na mwandishi Evans Magege.
Wengine ni Katibu Mwenezi wa CCM, Musoma Mjini, Fikiri Marumba na Ally Tesha ambao wote walipatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Kasulu na kuendelea na msafara.
Majeruhi mwingine ni Cyprian Msiba ambaye ni mwandishi wa kituo cha Televisheni cha Channel Ten ambaye alibaki hospitalini hapo kwa ajili ya huduma ya X-Ray kutokana na kuumia sehemu za bega.
Makongoro ambaye ni mbunge wa Afrika Mashariki, anazunguka mikoa mbalimbali nchini kwa nia ya kutafuta wadhamini ili kuomba ridhaa ya CCM kumpitisha kugombea nafasi ya urais.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 12011 Sep 20160
Tetemeko la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nc...Read more ?
- Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.09 Sep 20160
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao uliku...Read more ?
- Polisi Washuhudia Majambazi Yakitwangana Risasi.......Zakamatwa Shehena za Silaha na Vifaa vya Uhalifu06 Sep 20160
WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wa kutumia silaha, ambao wamehusika kufanya matukio ...Read more ?
- Askari Magereza Atiwa Mbaroni Kwa Kuingia Wodini Akiwa Amelewa na Kisha Kuanza Kufyatua Risasi28 Aug 20160
POLISI mkoani Rukwa inamshikilia askari Magereza, Cleophas Chapaulinge kwa kosa la kulewa na k...Read more ?
- Polisi Mwingine Auawa Kwenye Mapambano Makali na Majambazi Huko Mkuranga27 Aug 20160
Ilikuwa ni kama filamu ya askari na maadui wakati askari wa Jeshi la Polisi walipopambana na wat...Read more ?
- RC Makonda: Polisi Mkikuta Mtu Yeyote Msituni Pigeni bila Huruma.......Haki za binadamu Wakiwauliza Waambieni waje Kwangu26 Aug 20160
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameliagiza Jeshi la Polisi kuwagonga na kuwapiga wah...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment