Home
»
Entertainment
» TeamDiamond vs TeamAlikiba: Kinachoendelea Instagram kinatutia aibu watanzania!
Upinzani kati ya Diamond Platnumz na Alikiba sasa unaelekea kubaya. Kiukweli nimesikitishwa sana na kile ambacho ninakiona kikiendelea kwenye Instagram kati ya kambi hizi mbili.
Infact nahisi ushabiki huu una hasara nyingi kuliko faida kwenye industry yetu. Kwa leo sitaongelea jinsi ushabiki wa wasanii hawa wawili wenye nguvu unavyofanya wasanii wengine wanaofanya vizuri nchini kutoangaliwa, bali nitazungumzia kusikitishwa na kile kinachofanyika Instagram ambapo mashabiki wa Alikiba wameanzisha kampeni ya kuhakikisha kuwa Diamond anakosa tuzo kwenye MTV MAMA pamoja na mashabiki wa Diamond kumtukana Davido bila hatia!
Kwanini lakini tunafanya hivi? Hivi kweli tunaamua kujidhalilisha kiasi hiki? Majirani zetu wanatucheka, wanatubeza, wanatushangaa kweli kweli! Ushindani huu wa ndani kati ya wasanii hawa wawili kwanini uondoe utaifa wetu? Ushabiki gani huu?
Diamond Platnumz amechaguliwa kuwania vipengele vitatu kwenye tuzo za mwaka huu za MTV MAMA, iwapo akishinda, ushindi wake si wa familia yake na mashabiki wake peke yake, ni ushindi wa nchi nzima.
Kitendo kinachofanywa na maadui zake ambao infact ni mashabiki wa Alikiba na Wema Sepetu cha kuhamasishana kuwapigia kura Davido na Wizkid ili washinde na kumkomoa Diamond si kizuri.
Ni vyema linapokuja suala la kimataifa, tuweke tofauti zetu pembeni na tuwe kimoja. Kama hili haliwezekani, ni vyema kukaa tu kimya kuliko kuhamasishana kuwapigia kura wapinzani ili msanii wa Tanzania akose.
Haya, jana nimeshuhudia kitu kingine cha ajabu kabisa kwenye Instagram. Davido aliweka post kuonesha nominations nne alizopata.
From nowhere, comments nyingi zikawa ni kati ya Diamond vs Davido! Kwanini? Hii ni page ya msanii wa Nigeria ambaye anawataarifu mashabiki wake kuhusiana na nominations zake sasa huu ushabiki wa Diamond na yeye unatoka wapi tena?
Mbona tunatiana aibu kiasi hiki? Mbona tunaonekana malimbukeni na wageni wa mitandao? Hatuna kazi za kufanya ama nini hiki? Ndio, hadi wanaijeria wanatushangaa na kutuona kama wageni wa hivi vitu? Ugomvi wa Diamond na Davido ulishaisha siku nyingi sasa kwanini mashabiki wanalazimisha uendelee kuwepo?
Kama unampenda Diamond si unajua jinsi ya kumpigia kura, sasa kwanini uende kwenye page ya mtu ambaye wala hana time na masuala hayo na kuanza kumchafulia tu post yake?
Kiukweli tunatiana aibu. Tubadilike!
~Bongo5
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Diamond kuwania tuzo 5 za Afrima 2016, Alikiba na Yamoto Band moja08 Sep 20160
Diamond Platnumz ametajwa kuwania vipengele vitano kwenye tuzo za mwaka huu za Afrima. Vipeng...Read more ?
- Ujumbe wa Diamond kwa bintiye Wazua Gumzo......Kamwambia "Ukikua chonde mama ukitunze wasikile sana"23 Jul 20160
Diamond Platnumz si mgeni kwenye jumbe tata kwenye mitandao ya kijamii. Lakini ujumbe wake mpya...Read more ?
- Bifu Kali Kati ya Diamond na Clouds Media23 May 20160
Ni dhahiri sasa msanii wa kimataifa Diamond na brand kubwa ya radio na tv Clouds Fm, bifu la hadh...Read more ?
- Afande Sele Aungana Na Mbunge Joseph Msukuma Kuitaka Serikali Ihalalishe Matumizi Ya Bhangi02 Feb 20160
Msanii mkongwe wa hip hop nchini, Afande Sele amefunguka na kusema serikali ihalalishe matumiz...Read more ?
- Gari Jipya Analomiliki Masanja Mkandamizaji.10 Jan 20160
Msanii wa Vichekesho Anawakilisha kundi la Orijino Komedi anayejulikana kama Masanja Mkand...Read more ?
- Zari The Lady Boss Awakosha Mashabiki wa Penzi lake na Diamond Kwa Picha Hizi09 Jan 20160
Zari the Boss Lady ‘Mama Tiffah’ amewakosha mashabiki wa penzi lake na Diamond ‘Baba Tiffah’ baada...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment