March 17, 2025 02:10:42 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Image result for ULEVI
Mkuu wa Wilaya ya Rombo Lembris Kipuyo  amesema tatizo la ulevi kupindukia Wilayani humo limewaathiri wanaume kiafya na kuwataka watendaji kulivalia njuga. 

Kutokana na ulevi huo kuna madai kwamba baadhi ya wanawake wanaoishi kwenye ndoa wamelazimika kutafuta wanaume nchi jirani ya Kenya ili wapate mimba kutokana na wanaume zao kuzidiwa na ulevi hivyo kushindwa kuwahudumia.
Kipuyo alisema tatizo la ulevi limefikia hatua ya hatari zaidi na jitihada za haraka zinahitajika. 

Kipuyo alitaja maeneo yaliyokithiri kwa ulevi ni kilelewa ambapo ni mpakani mwa Tanzania na Kenya.
“Imefikia mahali wanaume wengi wanashindwa kumudu kufanya tendo la ndoa na kuwalazimu wanawake zao kukodi wanaume kutoka nchi jirani ya Kenya kwa ajili ya tendo hilo”Kapuya. 


Alisema ni vizuri mamlaka husika na Serikali ya vijiji kuhakikisha ulevi unakwisha ili kuepuka Wilaya hiyo kuwa na kizazi cha Wakenya.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
19 May 2015

Post a Comment

 
Top