Mkuu wa Wilaya ya Rombo Lembris Kipuyo amesema tatizo la ulevi kupindukia Wilayani humo limewaathiri wanaume kiafya na kuwataka watendaji kulivalia njuga.
Kutokana na ulevi huo kuna madai kwamba baadhi ya wanawake wanaoishi kwenye ndoa wamelazimika kutafuta wanaume nchi jirani ya Kenya ili wapate mimba kutokana na wanaume zao kuzidiwa na ulevi hivyo kushindwa kuwahudumia.
Kipuyo alisema tatizo la ulevi limefikia hatua ya hatari zaidi na jitihada za haraka zinahitajika.
Kipuyo alitaja maeneo yaliyokithiri kwa ulevi ni kilelewa ambapo ni mpakani mwa Tanzania na Kenya.
“Imefikia mahali wanaume wengi wanashindwa kumudu kufanya tendo la ndoa na kuwalazimu wanawake zao kukodi wanaume kutoka nchi jirani ya Kenya kwa ajili ya tendo hilo”Kapuya.
Alisema ni vizuri mamlaka husika na Serikali ya vijiji kuhakikisha ulevi unakwisha ili kuepuka Wilaya hiyo kuwa na kizazi cha Wakenya.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment