March 17, 2025 10:31:50 PM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Na Imelda Mtema
Beautiful Onyinye wa Bongo, Wema Sepetu amefunguka kuwa, anajua siku zote yeye hana bahati ya kuwa na marafiki kwa kuwa hata akiwa nao mwishowe kunatokea mgogoro na kuachana huku kila mmoja akimuona mbaya

Akizungumza na gazeti hili juzi, Wema alisema anaumia sana kwa kuwa mara nyingi anawapenda sana rafiki zake kwa moyo mmoja lakini mwisho wa urafiki wao huwa ni mbaya sana tena huvunjika kwa kugombana.

“Mimi nimeshajiona siku nyingi sina bahati kabisa, hata nikiwa na marafiki ambao nawapenda kutoka moyoni, mara nyingi wananigeuka na mama yangu amekuwa akinisihi mara nyingi sana, sasa naona bora nifuate ushauri ambao mama yangu ananishauri wa kuangalia watu wa kuanzisha urafiki nao,” alisema Wema.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
15 May 2015

Post a Comment

 
Top